Jina lake: TIBA HARUNA (miaka 29, mrefu wa futi 5)
amepotea kuanzia tarehe 27 Juni 2012.
Anaishi Buza kwa Mama Kibonge, Temeke.
TIBA anatatizo la akili na mara ya mwisho alikuwa amevaa sketi na blauzi ya batiki ya rangi ya Kijani na nyeupe, alifunga kilemba cheupe na khanga yenye maua ya njano.
TIBA amepotea na MWANAE WA KIUME - HARUNA (2) alikuwa amevaa fulana yenye mistari mieupe na bluu na kaptura yenye mistari miekundu.
Taarifa imetolewa kituo cha polisi Makangarawe Yombo IWAPO UTAMUONA YEYE AU MTOTO TUNAKUOMBA UTOE TAARIFA KITUO CHA POLISI KILICHO KARIBU AU WASILIANA NA:
Kijakazi M. Salim - 0754-891587
Mwanamtama M. Salim - 0768-359091
Mohamed N. Majembe - 0653-409909
Mohamed M. Mgomba - 0786-220815
Nashukuru kwa msaada wako, na M'Mungu atakulipa Inshaalah - Amin
NB: Picha inakataa ku-attach ingawa ina bites 4.0 hivyo naomba unielekeze nikufuate nikuletee picha tafadhali.
Mama Salim



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...