Waziri wa Fedha Dr. William Mgimwa akifungua mkutano maalum Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha leo jijini Dar es salaam . Katika salamu zake kwa wafanyakazi amewaagiza kuweka mfumo mzuri wa ulipaji mishahara ili kuepuka malipo kwa watumishi hewa na kuongeza kuwa watakaoshiriki katika malipo hewa watachukuliwa hatua kali.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanyakazi wa Wizara ya Fedha Ramadhan Khijjah akimkaribisha Waziri wa Fedha Dr. William Mgimwa (hayupo pichani) ili afungue mkutano maalum Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha leo jijini Dar es salaam.
Wajumbe wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi waandamizi wa Wizara hiyo mara baada ya ufunguzi wa mkutano maalum wa Baraza la Wafanyakazi leo mjini Dar es salaam.Picha na Tiganya Vincent-MAELEZO- Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. na joto lote amevaa sweta ndani. Kazi kweli...

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...