Serikali ya Australia itapeleka
kundi la wataalamu nchini Dubai kwa ajili ya kujadili njia za kuendeleza uchumi
unaofuata sheria za kiIslam nchini Australia. Ujumbe huo utakaongozwa na
mtaalamu wa kiuchumi wa Australia ndugu Barry O’Farrell na wataalamu wengine wa mambo ya kiuchumi,
watajadili maswala mazima yanayohusiana na usimamizi na sheria za uchumi huo,
wakati huohuo ujumbe huo utatembelea mji
wa Abu Dhabi na Lebanon.
Australia ina
mategemeo ya kua na mchango mkubwa ktk uchumi huo kwa kuzingatia kwamba nchi za
kusini mashariki mwa Asia ambazo zina uhusiano wa karibu na nchi hiyo, uchumi
unaofuata sheria za kiIslam unakua kwa kasi. Moja ktk matatizo yaliyopo ni pamoja
na uhakika kwamba juhudi za kupitisha sheria ya kuuruhusu uchumi huo kasi yake
ni ndogo sana ktk ngazi za juu, kitu ambacho kimeilazimisha serikali ya
Australia kuingilia kati. Serikali ya
Austaralia ina hamu kubwa ya kujihusisha na uchumi huo alisema Salim Farrar
muhadhiri mkuu wa kitengo cha
sheria ktk chuo kikuu cha Sydney ambae alikiri vilevile kwamba swala
hilo linahitaji mtiririko wa majadiliano ya kisiasa.
Pamoja na mambo
mengine Australia inakabiliana na changamoto zinazohusiana na sheria mpya za
uchumi unaofuata sheria za kiislam hususan ktk maswala mazima ya Islamic bonds
na triple tax duties. Kwa maelezo zaidi wasiliana na http://ijuebankyakiislam.blogspot.com



Ni habari njema kwa waislam na wsiokua waislam. Matatizo ya uchumi yanayoukumba ulimwengu yamesababishwa na vitu vingi ikiwemo riba, kutokua na uwazi uwazi ktk biashara nyingi, makisio ya faida yenye hatari kubwa yasiyolindwa na rasilimali na mengineyo kama vile kukataa kugawana hasara na faida ktk biashara na badala yake upande mmoja tu kubeba majukumu hayo peke yake. Ni wakati muafaka wa kuangalia njia mbadala za uchumi ambao unachunga sana maadili kuliko kuangalia faida tu.
ReplyDeletemtume muhammad hakika amesema ukweli na tunashuhudia.
ReplyDeleteSasa wamejua umuhimu wakufuata mfumo wakibiashara wakiislaam. Tatizo lakiichumi linaloikabili dunia pure inatokana na riba.
Uchumi wa Kiislamu,
ReplyDeletePana watu wana dhana potofu juu wa Uislamu na kupelekea kujenga chuki zisizo na msingi dhidi ya Uislamu kitu ambacho hakisaidii.
Kama kanunu za Kisayansi zimethibitisha Mfumo wa Kibenki na Uchumi wa Kiislamu ni suluhisho, je kwa nini binaadamu anapinga?