Kikao cha Uchaguzi cha Halmashauri ya Manispaa ya Nyamagana jijini Mwanza kimemchagua diwani wa Kata ya Mkolani Mh. Stanslaus Mabula wa CCM kuwa Meya wa jiji hilo mara baada ya kumshinda mshindani wake Charles Chinchibela wa CHADEMA aliyepata kura 8 ile hali Mabula akipata kura 11.
![]() |
| Ni picha ya pamoja Meya Mabula, mkuu wa wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga(katikati) na Naibu meya John Minja wakiwa katika ofisi ya Mstahiki Meya |
Ikumbukwe kuwa leo kulikuwa na chaguzi mbili za Ma- Meya na Ma- Naibu wake wa Halmashauri ya jiji la Mwanza (Nyamagana) na Manispaa ya Ilemela, baada ya uchaguzi wa Nyamagana kumalizika na wajumbe wake kuondoka ukumbini ili kuwapisha wajumbe wa wilaya ya Ilemela, nao waliketi katika ukumbi wa uchaguzi wakisubiri kushiriki uchaguzi wa kuteuwa Meya na Naibu Meya wao ambapo uchaguzi huo haukufanyika kufuatia diwani wa kata ya Kitangili kufungua kesi katika mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza kupinga kuvuliwa uanachama, kupinga kuenguliwa katika mchakato wa kuwania nafasi ya Meya hadi hapo uamuzi wa kesi yake utakapo tolewa, kutokana na kuwa na hati ya Mahakama inayomruhusu aidha kuruhusiwa kushiriki kupitia chama chake cha zamani (CHADEMA) au chama chake kutofanya uteuzi wa wagombea.
![]() |
| Madiwani wa CCM wilaya ya ilemela kabla ya uchaguzi wao kuahirishwa. |
![]() |
| Madiwani wa CHADEMA wakiwa na mbunge wao wa wilaya ya Ilemela Highness Kiwia (katikati) wakisubiri taratibu za uchaguzi ambao hata hivyo haukufanyika. |
![]() |
| Meya wa jiji la Mwanza (wa3kutoka kushoto) Naibu Meya (wa kwanza kushoto) wakiwa pamoja na Madiwani wa CCM wakimsikiliza mbunge wa viti maalum Maria Hewa (wa pili kutoka kulia) aliyekuwa akisema "Chama kimerudisha heshima yake katika jiji la Mwanza" Picha na habari na Libeneke la http://gsengo.blogspot.com/ |










CCM DUME!!!
ReplyDeleteCCM NYUNDO KUBWA !
NYIMBO ZA MIKOANI ZA CCM:
ReplyDeleteMTWARA:
1.NTANDAWILA EEE, EEEE
CHAMA CHA MAPINDUZI X 3
2.TUJENGE CHAMA EEE, EEE
CHAMA CHA MAPINDUZI X 3
.....(Repeat CHORRUS)
LINDI:
1.CCM INA NYUNDO NA JEMBE X 2
2.TANZANIA KOTE NCHINI MWETU YASIFIKA X 2
.....(Repeat CHORRUS)
RUKWA:
1.CCM PAMBALAMA X 2
2.POTELELI CCM, WEEE X 2,
3.POTELELI CCM PAMBALAMA X 1
.....(Repeat CHORRUS)