bondia Thomas Mashali akiwa na mikanda yake ya ubingwa wa Tanzania pamoja na wa Afrika Mashariki na Kati.
BONDIA THOMAS MASHALI kushoto akioneshana uwezo wa kutupiana masumbwi na  MEDY SEBYALA wa Uganda wakati wa mpambano wao wa kuwania ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati,uliofanyika kwenye ukumbi wa Friends Corner,Manzese jijini Dar .Katika mpambano huo Mashali alishinda kwa Point.
Bondia Medy Sebyala akioneshana ufundi wa kutupiana makonde na bondia Thomas Mashali wakati wa mpambano wao wa kugombea ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati. Mashali alishinda kwa point.
BONDIA THOMAS MASHALI kushoto akioneshana uwezo wa kutupiana masumbwi na  MEDY SEBYALA wa Uganda wakati wa mpambano wao uliofanyika kwa ajili ya kumbukumbu ya baba wa taifa Mashali alishinda kwa Point.
Bondia Medy Sebyala akioneshana ufundi wa kutupiana makonde na bondia Thomas Mashali wakati wa mpambano wao wa kugombea ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati Mashali alishinda kwa point.
KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Charles Kenyela kushoto akiwa amekinga ngumi huku akiwa na furahaa baada ya bondia Thomas Mashali kuibuka na ubigwa kwa kumpiga bondia kutoka Uganda wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya baba wa taifa.
Bondia Thomasi Mashali akiwa na mkanda wake wa ubingwa wa Afrika Mashaliki katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali.
Mbunge wa Kinondoni Iddy Azani akiwa katika picha na Bondia Thomas Mashali baada ya kuvishwa ubingwa wa Afrika Mashariki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Hureeeeee!

    Wajameni tutakuwa tumemkosea nini Mwenyezi Mungu?

    Kila kitu tushindwe hadi magumi ambayo tupo vizuri tu hata kwa street fighting?

    Hongera sana Mwanandugu Thomas Mashali kwa kumchapa Mganda, nimefurahi sana maana jamaa alikuwa na nyodo na juzi kati ile kabla ya Pambano alitamba sana!

    ReplyDelete
  2. Ahsante sana Bwana Kaka Thomas Mashali kwa kumchapa Muganda!

    Umetutoa kimaso maso wa Tanzania wote kwa kumkata Mganda ngebe zake!

    ReplyDelete
  3. Chezea Tanzania weye?

    Ulikuwa hujui wa-Tanzania akiwemo THOMAS MASHALI ni ngumi jiwe?

    Nenda ukalie kilio kwa mama yako kwenu Uganda akuchemshie maji na mapumba akukande kwa kupunguza maumivu!

    ReplyDelete
  4. TANZANIA NYUNDO KUBWA!

    Mganda unacheza na Mtanzania?

    ReplyDelete
  5. Safiiii saaaaana!

    Ahsante sana Thomas Mashali kwa kuibeba vizuri Bendera ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!

    ReplyDelete
  6. Shukrani sana Bondia Thomas Mashali!

    Vita uliyopigana kwa kumweka chali Mganda huyo ni sawa na Vita ambayo Raisi Jakaya kikwete muda si mrefu (Sio kwa vita bali kwa njia ya Sheria na Hoja za Mahakama za Kimataifa) atamweka chali mwana mama Raisi wa Malawi Joyce Banda kwa kudai Ziwa Nyasa lote ni la kwao!

    ReplyDelete
  7. Hongera sana Wapiganaji wa Kitanzania!

    Baada ya

    1.Thomas Mashali kumlaza chali Mganda,

    2.sasa tunasubiri kwa hamu kubwa Bondia Maarufu Raisi JK kumchapa kwa KNOCK OUT Raisi king'ang'anizi wa Malawi mama Joyce Banda anayedai Ziwa Nyasa!

    TUNA MATUMAINI MAKUBWA KWA KUWA TUMEONA KULE UMOJA WA MATAIFA MAREKANI KWENYE KIKAO ULIMFUNIKA KABISA KIASI RAISI JOYCE BANDA WA MALAWI AKAPANDA JAZBA NA SASA ANAELEKEA KULIPELEKA SUALA MAHAKAMA YA DUNIA AMBAKO TUNAAMINI KIONGOZI WETU JK UTAMGARAGAZA PIA!

    ReplyDelete
  8. Hongera kwa kuleta heshima nyumbani, jitahidi mwanzo mzuri.

    ReplyDelete
  9. Tusiishie kuwa wakali wa kuwachapa wapinzani wetu Majukwani kwenye ngumi wa Tanzania tuwe Mabondia wakali pia kwa kuilinda Mipaka yetu kama hili suala linalotia ghadhabu sana la Ziwa Nyasa na Malawi!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...