Timu ya katonga A ambao ni mabingwa wa mkoa wa Kigoma wakimaliza mashindano ya kupiga makasia ya Bia ya Balimi kwenye Ziwa Tanganyika.
Meneja wa Bia ya Balimi Edith Bebwa kulia akishuhudia namna wachezaji wa timu mbalimbali walivyokuwa wakitoana jasho kwenye fainali ya Mashindano ya Kupiga makasia ya Bia ya Balimi kwenye ziwa Tanganyika.
Mabingwa wa mashindano ya Balimi boat race mkoa wa kigoma upande wa
wanaume Timu ya Katonga A wanaume wakishangilia mara baada ya kuwa
mabingwa wa mkoa huo na kukabidhiwa jumla ya shilingi laki tisa kama
zawadi ya ushindi wa kwanza.
Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh Ramadhani Maneno akimkabidhi kitita cha Shilingi laki saba kepteni wa timu ya wanawake ya upendo bi mawazo shaban Juhudi mara baada ya kuibuka kidedea kwenye fainali hiyo.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...