Naibu Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria, Angela Kairuki akiwasalimia Maofisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakati alipofanya ziara ya kikazi leo katika Gereza la Keko lililopo jijini Dar es Salaam.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria, Angela Kairuki akionja chakula cha Mahabusu na Wafungwa wa Gereza la Keko lililopo jijini Dar es Salaam alipotembelea sehemu ya jiko la Mahabusu na Wafungwa gerezani hapo leo.

 Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akimkaribisha Naibu wa Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria, Angela Kairuki (wa pili kushoto) azungumze na Maofisa wa Magereza katika ziara ya Kikazi aliyoifanya leo Gereza la Keko lililopo jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria, Angela Kairuki akizungumza na Mahabusu na Wafungwa (hawapo pichani) wa Gereza la Keko jijini Dar es Salaam alipofanya ziara ya kikazi gerezani hapo leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...