Na Veronica Kazimoto –
MAELEZO
Sikukuu ya Eid-El-Hajj
itakuwa siku ya tarehe 26 Ockoba mwaka huu ambapo kitaifa swala itafanyika
katika msikiti wa Vuchama, wilayani Mwanga, katika mkoa wa Kilimanjaro, ikifuatiwa
na Baraza la Eid baada ya Swala.
Kwa mujibu wa taarifa
ya Mkurugenzi wa habari na mawasiliano ya Umma Simba Shabani wa Baraza Kuu la Waislam
wa Tanzania (BAKWATA) mgeni rasmi anatarajiwa kuwa kuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano
wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete.
Taarifa hiyo imefafanua
kuwa sababu ya tarehe hiyo ni kutokana na siku hii ya leo kuwa mwezi pili,
Dhul-Hijja mwaka 1433 kwa mujibu wa kalenda ya Kiislam.
Aidha Mufti na Sheikh Mkuu
wa Tanzania Issa Bin Shaaban Simba amewataka Waislam wote nchini kusherehekea
kwa amani na utulivu sikukuu hiyo huku wakichunga mipaka ya Allah (S.W).
Sheikh Shaaban Simba
pia amewataka waislamu kutii sheria za nchi na kuepukana na watu ambao wanataka
keleta tafrani za kidini hapa nchini.
Vuchama Ugweno au,maana Mwanga kuna Vuchama ya Ndambwe.
ReplyDeleteTunaomba ufafanuzi.
Eid inatarajiwa kuswaliwa hiyo Ijumaa ijayo 26 Oktoba wakati Waislamu wakiwa Lupango na wengine hawajulikani walipo!
ReplyDeleteHivi tunakwenda wapi?