Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawatangazia wananchi wote kuwa sasa huduma ya kumpatia mteja huduma ya umeme imeboreshwa zaidi.

Wananchi wote ambao hawajapata huduma hii ya nishati ya umeme; hasa wale wanaoishi maeneo ambayo tayari kuna miundombinu ya TANESCO, wakilipia wanapatiwa huduma hii ndani ya wiki mbili tu.

Wateja wote wapya wanashauriwa wafike ofisi za TANESCO zilizokaribu nao kwa ajili ya kuomba kupatiwa na kulipia huduma hii ya umeme.

Kwa maelezo zaidi au tatizo lolote tafadhali fika ofisi ya TANESCO iliyo karibu nawe na umuone meneja wa mkoa au wa wilaya au wasiliana nasi kwa simu namba:

+255 767 902 312- Inj.Sophia S. Mgonja- Meneja Mwandamizi
                              Usambazaji
+255 782 222 996- Inj.Simon Kihiyo - Meneja Utekelezaji Usambazaji
+255 754 266 257- Inj.Seleman Mgwira - Mhandisi Mwandamizi
                              Usambazaji

Tahadhari: Epuka kudanganywa na Vishoka,fanya malipo yako yote kwenye
Ofisi ya TANECSO.

        TANESCO TUNAANGAZA MAISHA YAKO.

Imetolewa na:         
Ofisi ya Uhusiano

                               Tanesco -  Makao Makuu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...