Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule, akipokea Ujumbe Maalum kutoka Serikali ya Argentina kwa niaba ya Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kutoka kwa Balozi Bibiana Jones. Balozi Jones ni Mkurugenzi wa Idara ya Afrika anayeshughulikia nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Argentina.


Bw. Haule akizungumza na Balozi Jones mara baada ya kupokea Ujumbe Maalum.

Balozi Jones akifafanua jambo kwa Bw. Haule wakati wa mazungumzo yao.

Katibu Mkuu, Bw. Haule akiendelea na mazungumzo na Balozi Jones kuhusu ushirikiano baina ya Tanzania na Argentina. Mwingine katika picha ni Balozi Dora Msechu, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. huyo muangentina ni Mkurugenzi Idara ya Afrika anayeshughulikia Afrika kusini mwa jangwa la Sahara wakati sisi Amerika na Ulaya ni Kurugenzi moja!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...