Muimbaji mahiri wa kike hapa nchini Judith Wambura (kulia) almaarufu kwa jina la Lady Jay Dee akizungumza na waandishi wa habari leo katika mgahawa wake wa ‘Nyumbani Lounge’ uliopo jijini Dar es Salaam na kutambulisha rasmi kipindi chake kipya cha luninga kitakachoitwa‘Diary ya Lady Jay Dee’.
Amesema madhumuni ya kipindi hicho ni kuleta burudani tofauti kwa wapenzi wa muziki wake na muziki wa kizazi kipya kwa ujumla, vilevile kitatoa fundisho na changamoto kwa wasanii chipukizi kujua wasanii wakongwe wamepitia katika vikwazo gani.
Lady Jay Dee amesema kipindi hicho kitaonyeshwa ndani ya East Africa Television kuanzia tarehe 18 Novemba mwaka huu kila siku ya Jumapili.
Aidha ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa makampuni mbalimbali kujitokeza kushiriki katika kudhamini vipindi vinavyobuniwa kama hivyo ili kuweza kutoa ajira kwa wasanii na wadau wengine wa sekta ya muziki na burudani.Kushoto ni Mkuu wa Vipindi wa East Africa TV Bi. Lydia Igarabuza
Mkuu wa Vipindi wa East Africa TV Bi. Lydia Igarabuza akizungumzia jinsi stesheni hiyo ilivyopokea kwa shangwe kipindi hicho na kuwa kitakuwa hewani Jumapili saa 3 usiku kuanzia Novemba 18 na kuwataka vijana wa Afrika Mashariki kukitazama ili kujifunza mengi kutoka kwa watu ambao tayari wanamafanikio kupitia tasnia ya muziki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Du lydia umri unakwenda nikikumbuka enzi hizo ulikua moto kinoma na napenda style yako ya u simple bado unaendeleza, poa kila la heri.

    ReplyDelete
  2. another talk show??

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...