Mwalimu Mboya akisindikizwa na walimu wenzake wakitoa  msaada wa ndala dazani moja, dawa za mswaki dazani mbili na miswaki dazani mbili. Kuanzia kushoto ni Mwalimu Ana Kimatare, Mzee Hamisi Mwakimwagile (akiyepokea msaada huo kwa niaba ya Tanzania 50 Plus Campaign), Mwalimu Florence Mboya, Mwalimu Happy Lumbwe na Mwalimu Ng’walu Mipawa.

Tanzania 50 Plus Campaign ikishirikiana na waathirika  wa saratani na marafiki wa kampeni itatembelea hospitali ya wagonjwa wa saratani katika hospitali ya Ocean Road Cancer Institute tarehe 24 Novemba 2012 saa 4 asubuhi. Ili kufanikisha zoezi hilo imeomba watu binafsi na makampuni mbali mbali na jamii kwa ujumla kuchangia misaada ya sabuni za kufulia, za kuogea, mafuta ya kujipaka (petroleum jelly), miswaki, dawa za miswaki, ndala, maji ya kunywa, juice mbalimbali na mtunda.

Tanzania 50 Plus Campaign inamshukuru sana Mwalimu Florence Mboya kwa ukarimu wake na moyo wa upendo na huruma kwa wale wenye mahtaji. Bado tunaendelea kupokea misaada. 
Ukiwa na msaada wako wasiliana nasi:
Simu  0754 402033 

au barua pepe: chrptz@yahoo.com,
 ekandusi@yahoocom

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...