Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule akizungumza na Mhe. Flosie Gomile Chiyaonga, Balozi wa Malawi hapa nchini kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Timu ya Pamoja ya Wataalam wa Tanzania na Malawi kuhusu mgogoro wa mpaka kwenye Ziwa Nyasa.


Bw. Abdallah Mtibora, Afisa kutoka Kitengo cha Sheria, Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Kimataifa akimkaribisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kufungua mkutano huo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule, akifungua Mkutano wa Timu ya Pamoja ya Wataalam kati ya Tanzania na Malawi kuhusu mgogoro wa mpaka kwenye Ziwa Nyasa. Mkutano huo uliowahusisha wataalam kutoka Wizara na Idara mbalimbali za Serikali za Tanzania na Malawi unafanyika  Jijini Dar es Salaam katika Hoteli ya Serena.

Baadhi ya Wajumbe kutoka Malawi wakimsikiliza Katibu Mkuu (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.                 
Bw. Julius Chisi, Naibu Mpimaji Ardhi Mkuu kutoka Malawi  akizungumza machache wakati wa mkutano huo.

Baadhi ya Wajumbe kutoka Tanzania akiwemo Mhe. Balozi Patrick Tsere (wa pili kutoka kushoto), Balozi wa Tanzania nchini Malawi na Balozi Irene Kasyanju (kushoto) wakimsikiliza Bw. Chisi (hayupo pichani) wakati wa akizungumza.

Baadhi ya Wajumbe wengine kutoka Malawi akiwemo Mhe. Chiyaonga (kulia), Balozi wa Malawi hapa nchini.

Sehemu nyingine ya Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo.   

Picha na Habari na Rosemary Malale
Mkutano kati ya Tanzania na Malawi kujadili suluhu ya mgogoro wa mpaka kwenye Ziwa Nyasa umeanza katika ngazi ya Wataalamu jijini Dar es Salaam tarehe 15 Novemba, 2012.

Mkutano huo unaowahusisha wataalam kutoka Wizara na Idara mbalimbali za Serikali za Tanzania na Malawi unafanyika Jijini Dar es Salaam katika Hoteli ya Serena.

Akifungua Mkutano huo Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule alisisitiza umuhimu wa wajumbe kutoka nchi zote mbili kujadili na kupendekeza njia zitakazosaidia kupata suluhisho la kudumu la mgogoro huo.

Aidha, Bw. Haule aliweka bayana kuwa Serikali ya Tanzania ina dhamira ya dhati kufanya kazi pamoja na Serikali ya Malawi kutafuta suluhu ya mgogoro huo jambo ambalo pia lilisisitizwa na Bw. Julius Chisi, Kiongozi wa Ujumbe wa Malawi.

Mkutano huo ambao utafanyika kwa siku tatu hadi tarehe 17 Novemba, 2012 umeanza na Kikao cha Wataalamu ambacho kitafuatiwa na kikao cha Maafisa Waandamizi na kuhitimishwa na kikao cha Mawaziri tarehe 17 Novemba, 2012.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Licha ya hoja za uhakika zenye kupambwa na uthibitisho wa nguvu tunatumia uwanja wa nyumbani lazima tushinde mechi hii na kumaliza utata na kukunja safu hii ya mzozo.
    kila la heri wadau.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...