Na Mwandishi Maalum

Tanzania imeshauri na kupendekeza kwamba, mkutano wa 57 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya Wanawake, (CSW57) pamoja na mambo mengine ujielekeze zaidi katika kuhakikisha kwamba ahadi ambazo zimekwisha kutolewa zinazolenga kumkomboa mwanamke dhidi ya ukatili vit zinatekelezwa.

Ushauri huo umetolewa na Balozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Tuvako Manongi, wakati wa mkutano wa siku mbili wa maandalizi ya Mkutano wa 57 wa CSW utakaofanyika kuanzia tarehe 4 hadi 15 Marchi mwaka 2013.

Ahadi ambazo Tanzania inataka zitekelezwe ni pamoja ile ya kuwapatia fursa ya elimu wanawake na watoto wa kike. Kwa kile ambacho, Mwakilishi huyo wa Tanzania amesema ni moja ya nyezo muhimu za kuliwezesha kundi hilo la jamii kukabiliana na kuepukana na aina zote za ukatili dhidi yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...