*Asema kama niliweza TFF siwezi kushindwa
TOC
*Aahidi ushirikiano wa karibu na Serikali,
wadau wa michezo
*Ashangaa kukosekana kwa medali za Olimpiki
tangu 1980
*Aahidi uwazi kwenye mapato na matumizi ya
TOC
SIKU chache baada ya kupitishwa kugombea
nafasi ya Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki ya Tanzania (TOC), Katibu Mkuu wa
zamani wa Shirikisho la Soka nchini (TFF) Frederick Mwakalebela amezindua
kampeni zake kwa kishindo na kuahidi kurejesha heshima ya nchi kwenye michezo
kimataifa.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini
Dar es Salaam, Mwakalebela alisema ni aibu kwa nchi yenye idadi ya watu
zaidi ya milioni 40 na vipaji kibao kama Tanzania kukosa medali kwenye michezo
mikubwa kama ya Olimpiki kwa zaidi ya miaka 30 sasa.
“Olimpiki ni mashindano makubwa
yanayojumuisha michezo mbalimbali, lakini tangu mwaka 1980, pamoja na kupeleka
wanamichezo kwenye mashindano hayo, hatujawahi kupata medali hata moja,”
alisema.
Akiwa
makini kutopeleka lawama kwa uongozi wa TOC uliopita, Mwakalenela alisema
kilichosababisha kupatikana kwa medali mwaka 1980 huko Moscow, Urusi (USSR) ni
mfumo mzuri wa maandalizi ya timu ambapo timu hiyo ilifanya maandalizi ya mwaka
mzima kwa kufanya ziara mikoani na nje ya nchi.
“Kwanini siku hizi inashindikana kufanya
hivyo? Ni ukosefu wa ubunifu, na ndio maana ninagombea ili kuleta mawazo mapya
michezoni. Nikiingia ofisini kazi yangu ya kwanza itakuwa ni kuiweka TOC karibu
na wadau wakubwa wa michezo ambao ni Serikali, vyombo vya habari, makampuni ya
biashara, majeshi, shule, vyuo na taasisi mbalimbli binafsi.
“Ndani ya miezi mitatu tu wadau hao
watakuwa ‘marafiki’ wa TOC na maandalizi ya michezo ya Olimpiki ya mwaka 2016
huko Rio de Janeiro, Brazil yataanza mara moja. Tukikosa medali mwaka huo, basi
ni lazima tutapata mwaka 2020,” alisema kwa kujiamini.
Akijibu maswali mbalimbali ya waandishi,
Mwakalebela aliyefanya kazi kwa ufanisi mkubwa akiwa TFF, alisema TOC mpya
itakaa na Rais Jakaya Kikwete na kumwomba kabla hajamaliza muda wake wa uongozi
serikalini awaachie wanamichezo wa Tanzania kumbukumbu ya Kijiji cha Olimpiki.
Alisema kuwapo kwa kijiji hicho kutawapa
nafasi vijana wenye vipaji nchini kuonyesha uwezo wao na kutokana na wao, ndipo
timu bora ya taifa itakayokuwa ikiiwakilisha nchi kwenye michezo mbalimbali
itakuwa ikipatikana.
“Tutashirikiana na wizara husika, balozi za
kimataifa, Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGOs) yanayotoa nafasi za mafunzo
(scholarship awards) na organaizesheni za michezo za kimataifa kuwatafutia
wanamichezo wetu nafasi za masomo na mafunzo nje ya nchi.
“Hili liwahi kufanyika na watu kama kina
Filbert Bayi, Suleiman Nyambui na Mwinga Mwanjala walifaidika sana na mpango
huu na kisha kuliletea taifa letu sifa kubwa michezoni,” alisema Mwakalebela
ambaye kwenye kinyang’anyiro hicho atapambana na Bayi anayetetea nafasi ya
Katibu Mkuu wa TOC.
Kikubwa zaidi, Mwakalebela alisema mapato
na matumizi ya TOC yatawekwa wazi ili kile kidogo kinachopatikana,
kikijumlishwa na kingine kutoka serikalini na kwa wadau, kifanye kazi
iliyokusudiwa ya kuendeleza michezo nchini.
TOC ndio msimamizi na mlezi wa vyama na
mashirikisho ya michezo nchini na ndio waandalizi wa timu za taifa
zinazoshiriki michezo ya Olimpiki, Jumuiya ya Madola na Michezo ya Afrika (All African
Games).
Haya bwana. Nimewahi kuskia bwana huyu akiwa huko TFF na ilitokea nini cjui hayuko huko tena.
ReplyDeleteOk labda tumpe nafasi huku TOC kwa kauli zake hizi nzuri zinazoyapendeza masikio yetu.... Hata mkosaji aweza pewa nafasi ya pili. Nashauri haya aliyoyasema hapa yachapwe na kuwekwa kwenye mbao za matangazo huko afisi za Olimpki na iwe dira na angalizo nyakati za utendaji wake. Na siye Wadau bila kupepesa mimacho tuje tumwuulize Pale atakapo kiuka aliyoyaimba leo. Else Tumpongeze endapo atatufikisha kunako nozi zake na zilizo za wengi pia.Isijekuwa mvinyo mupya chupa ileiile! God Bless Us All
Huyu nadhani anaweza nimeuona uso wake unaeleza kuhusu moyo wake, mpeni atafanya kweli.
ReplyDeletekule TFF hakukosea chochote ila aliacha mwenyewe ili kwenda kugombea ubunge huko Iringa ambako alikumbwa na kashfa ya rushwa!!! anafaa tumpe nafasi atuletee mageuzi TOC
ReplyDelete