Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana Zahor Kassim Mohamed EL-KHAROUSY kuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi katika Bahari Kuu.
Taarifa iliyotolewa na kutiwa saini leo, Ijumaa, Desemba 7, 2012 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue inasema kuwa uteuzi wa Bwana El Kharousy ulianza Novemba 28, mwaka huu, 2012.
Kabla ya uteuzi wake, Bwana Kharousy alikuwa Naibu Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
7 Desemba, 2012
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...