Wizara ya Ujenzi inapenda kutoa taarifa kwa Umma kwamba, Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dk. John Pombe Magufuli (Mb) kwa Mujibu wa kifungu Na.3 (3), cha Sheria ya Usajili wa Makandarasi namba 17 ya mwaka 1997 pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2008,  amefanya uteuzi wa Wakurugenzi wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi. Uteuzi huu unafuata kumalizika kwa kipindi cha Bodi iliyotangulia tarehe 30/11/2012.  Katika uteuzi huu, Waziri  amemteua Eng. Consolatha Ngimbwa kuendelea kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB). Eng. Ngimbwa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Electrics International Co. Ltd.

Wakati huohuo, Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dk. John Pombe Magufuli (Mb) ameteua wajumbe nane (8) wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi  kama ifuatavyo:-
  1. Qs. Joseph Tango kutoka Tanzania Institute Quantity Surveyors (TIQS). Kwa sasa  Qs. Tango ni Makamu Mwenyekiti wa TIQS.
  2. Eng.Samuel D. Shilla kutoka  Association of Consulting Engineers  Tanzania  (ACET). Kwa sasa Eng. Shilla ni Mkurugenzi Mtendaji wa Service Consult Ltd.
  3. Eng. Lawrence Mwakyambiki kutoka Chama cha Makandarasi Tanzania. Kwa sasa ni Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wakandarasi na Mkurugenzi Mtendaji Mac Contractors Ltd.
  4. Eng. Stephen P. Makigo kutoka Chama cha Makandarasi Tanzania. Kwa  sasa ni Mkurugenzi Mkuu wa Manyanga Company Limited.
  5. Mr. Andrew Willson  Masawe, akiwakilisha Sekta ya Biashara.
  6. Eng. Joseph M. Nyamhanga, Mkurugenzi wa Barabara, Wizara ya Ujenzi.
  7. Mr. Abraham Senguji, Mkurugenzi wa Usuluhishi na Upatanishi, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
  8. Arch. Dudley B. Mawala, Mkurugenzi Mtendaji (Md Consultancy Limited). Anawakilisha Architectural Association of Tanzania (AAT). 
                                Uteuzi huu umefanyika tarehe 13/12/2012. Jukumu la msingi la Bodi ya Makandarasi ni kusajili Makandarasi; kusimamia mwenendo wa Makandarasi; kujenga uwezo wa Makandarasi wa Kitanzania na kulinda maslahi ya watumiaji wa Makandarasi.
                                                    Taarifa hii imetolewa na:

Balozi Herbert E. Mrango
KATIBU MKUU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hongera Eng. Consolatha Ngimbwa. Nakuomba kabla ya kumaliza muda wako huu, ujitahidi kwa udi na uvumba ku wezesha utaratibu wa kuwa na Quota >30% ya wanawake Engineers wenye uwezo kuteuliwa kuwa wajumbe katika Bodi ijayo.Wale uliyo wa mentor waje juu!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...