Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana Zahor Kassim Mohamed EL-KHAROUSY  kuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi katika Bahari Kuu.


Taarifa iliyotolewa na kutiwa saini  na Ijumaa, Desemba 7, 2012 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue inasema kuwa uteuzi wa Bwana El Kharousy ulianza Novemba 28, mwaka huu, 2012.

Kabla ya uteuzi wake, Bwana Kharousy alikuwa Naibu  Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
7 Desemba, 2012


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ukisoma jina tu, unaweza kuuvaa mkenge na kufikiri jamaa ni mwarabu! shabaash, kumbe ni mpingo wa nguvu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...