Waziri Mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa akitoa pole kwa mama mzazi wa Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana CCM,Marehemu Benson Mollel aliyefariki dunia katika mazingira ya kutatanisha katika hoteli moja jijini Arusha.
Waziri Mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli,Mh. Edward Lowassa akiwapa pole baadhi ya ndugu na jamaa wa marehemu Benson Mollel wakati alipofika nyumbani kwa Marehemu,Daraja Mbili Jijini Arusha jana.
Waziri Mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa akiwa na mwenyekiti wa CCM Monduli Ruben Kunei (kulia) na mjumbe wa halmashauri kuu taifa NEC Mathias Manga (kushoto) wakati walipohudhulia msiba huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...