Katika nchi ya Tanzania zimekuwepo jitihada nyingi kuongeza upatikanaji na utumiaji wa Nishati jadidifu.Kwa muda mrefu sasa kumekuwa hakuna utaratibu maalum unaoonyesha ukusanywaji wa taarifa juu ya hali halisi ya maendeleo ya sekta ya Nishati jadidifu kama ilivyo katika sekta nyingine mathalani Afya.

Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na Taasisi ya wadau wa nishati Jadidifu nchini Tanzania(TAREA) wameandaa warsha ambayo wadau mbali mbali wa Nishati watabadilishana mawazo juu ya hali halisi ya Teknolojia ya Nishati jadidifu nchini Tanzania hadi kufikia mwezi Disemba 2002

Mwishoni mwa warsha hii,washiriki watatoa maoni yao juu ya mfumo na mbinu za kuendeleza ukusanyaji taarifa kuhusu maendeleo ya Teknolojia ya Nishati jadidifu.

Katika warsha hii COSTECH na TAREA watabadilishana makubaliano ya ushirikiano kati yao juu ya mambo yote yanayohusu utafiti,uhawilishaji na ukuzaji wa teknolojia ya nishati jadidifu.
MKURUGENZI MKUU WA COSTECH DR HASSAN MSHINDA AKIONGEA NA WAANDISHI WA HABARI JUU YA MAKUBALIANO YA COSTECH NA TAREA KATIKA UTAFITI,UHAWILISHAJI NA UKUZAJI WA TEKNOLOJIA YA NISHATI JADIDIFU.
WASHIRIKI KATIKA WARSHA HIYO.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...