Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza Bibi. Margaret Thatcher maarufu kama "Iron Lady" amefariki dunia leo akiwa na umri wa miaka 87. 

Watoto wa marehemu Sir. Mark na Bint Carol wamethibitisha kuwa mama yao Margaret (Baroness) Thatcher amefariki leo asubuhi na alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa "Stroke". 

Marehem Margaret Thatcher alikuwa waziri mkuu wa Uingereza kuanzia 1979-1990, katika kipindi cha utawala wake alikuwa akilumbana sana na nchi changa zinazoendelea kwa ajili ya kuvutia maslahi ya Uingereza,kitu ambacho viongozi wa nchi nyingi za jumuiya ya madola hawakukubaliana naye.

Lakini kwa nchi yake atakumbukwa kuwa ni kiongozi aleyesaidia sana kunyanyuka kwa uchumi wa Uingereza katika enzi za utawala wake. 

Habari zaidi zitafuata baadaye

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Tangulia kwa amani mama Thatcher.Poleni waingereza kwa kumpoteza mama huyu.

    Kipindi anatawala uingereza,kule marekani kulikuwa na Reagan,na kule Africa ya kusini kulikuwa na kaburu Botha ,watatu hawa misimamo yao kwa mtu mweusi ilikuwa haipishani walikuwa kinyume kabisa na mtu mweusi.

    ReplyDelete
  2. Jana katika mitaa ya UK walikuwa wakisheherekea kifo cha "Iron Lady"!!

    ReplyDelete
  3. RIP
    Here in ma country we neither have Iron ladies nor Iron men. Most of those supposed to show the way are bagasse! or midebwedo. No rule of law.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...