Kutoka kushoto ni Kaimu Afisa Masoko Bodi ya Korosho,Bi Theophina Nyoni,Kaimu Katibu tawala Mkoa wa Lindi,John Likango na mwisho ni Mwenyekiti wa Ilulu Union Killian Kapamba wakiongoza kikao cha Wakulima wa zao la Korosho,Mkoani Lindi.
Wadau mbalimbali wa zao la korosho wakiwemo wenyeviti wa Halmashauri na Amcos za mkoa wa Lindi wakiwa katika kikao ambacho kilitoa maadhimio ya kuuzwa kwa korosho kilo Milioni 17 zilizo ghalani kwa bei yote itakayoletwa na mnunuzi huku Mkulima atoweza kulipwa kama alivyohaidiwa.

WAKULIMA wa korosho mkoani Lindi wamekubali kuuza korosho zao chini ya bei ya dira 1200 iliyotangazwa na bodi ya korosho mwanzoni mwa msimu mwaka huu.

Makubaliano hayo yalifanyika baada ya Kaimu Afisa masoko wa Bodi ya korosho Tanzania,Bi Theophina Nyoni kutoa maelezo juu ya mwenendo wa bei ya korosho katika soko la Dunia ambayo inaonyesha kushuka badala ya kupanda.

Kikao hicho kilichojumuisha wadau mbalimbali wa zao hilo wakiwemo viongozi wa vyama vya ushirika vya msingi,Wenyeviti wa Halmashauri za wilaya za, Mkoa wa Lindi na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Lindi Frank Magali,na kufanyika katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa.

Nyoni alisema serikali iliweka bei dira 1200 kwa kila kilo moja ya korosho ikitegemea soko la litapanda lakini hivi sasa limekuwa likishuka siku hadi siku kutoka 2800 kwa kilo moja hadi 2200 kwa sasa ambayo hawezi kukidhi kumlipa mkulima shs 1200 kutokana na gharama za uendeshaji pamoja ushuru wa Halmashauri ulio kisheria.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa chama cha msingi Umoja wilaya Liwale Hasani Mpako aliwataka viongozi wa Bodi ya korosho Pamoja na Serikali kutambua kuwa wakulima wa mikoa ya kusini utegemea zao hilo kuendesha maisha yao hivyo basi kushuka kwa bei hiyo ni kuhatarisha maisha ya wananchi hao.

Mpako alisema kutoka na hilo ni wajibu wa serikali kulipia hasara wanayoipata wakulima kwa kuuza korosho zao chini ya bei dira 1200 ambayo ilitangazwa na bodi ya korosho.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, John Likango ambae ndie Mwenyekiti wa kikao hicho alisema kuwa kikao cha pamoja kati ya wakulima, bodi ya korosho na sekretieti ya mkoa pamoja na wadau wengine kilipitisha maazimio mawili la kwanza wakulima kwa pamoja wamekubali kuuza korosho zote kilo milioni 17,600 kwa bei yeyote itakayopatikana kwa makampuni ya ununuzi.

Likango alisema azimio hilo limejitokeza baada ya kuona hali ya soko la dunia la zao hilo kuwa tete kwa kuyumba mara kwa mara kutoka shs 2800 hadi 2200 kwa sasa.

Hata hivyo kikao hicho ambacho pia kilienda kwa malumbano,Wakulima waliadhimia kuchangishana ili Tume waliyoiunda kwenda Ikulu kuonana na Rais Jakaya Kikwete kufuatia kukosa Imani na Bodi hiyo ikiwa pamoja na kutotekelezwa kwa Maagizo yake aliyoyatoa katika ziara yake Mkoani Lindi na kukutana na Wadau Wilayani Kilwa mwishoni mwa mwaka jana

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Wakati wa kuteremka kwa mfumo wa hela duniani, wanunuzi wa pamba walilalmika kuwa hawataweza kuyalipa mabenki walikokopa mihela.

    Serikali ilikimbia hima kuyalipa mabenki hayo mamilioni na mamilioni!

    Sijui hizo benki zilikuwa za wa-Tanzania au za nchi za nje?

    Yaani umma ulipi mabenki ya nje pesa zake na iache kuwalipa wananchi wenyewe?

    Acha mabenki yafilisike; ndio uchumi wa ki-bepari huo!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...