Mwenyekiti wa Chama cha CUF, Mheshimiwa Profesa Ibrahim Lipumba amekaririwa na Gazeti la Mwananchi la leo, Jumatano, Mei 15, 2013 akisema kuwa “amenasa taarifa za siri za kuwepo kwa mipango ya kuongeza muda wa Serikali ya sasa kukaa madarakani”.
Katika habari hiyo iliyoandikwa chini ya kichwa cha habari, “Lipumba: Kuna njama za kumwongezea JK muda” Mheshimiwa Lipumba anadai kuwa Serikali ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete “ itakaa madarakani hadi mwaka 2017”  kwa sababu kuna “wasiwasi kuwa mchakato wa sasa wa kupata Katiba Mpya hautaweza kukamilika mwaka 2014.”
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, inapenda kufafanua kuwa taarifa hiyo ya Mheshimiwa Prof. Lipumba ni uzushi mtupu na ni upotoshaji usiokuwa na msingi.  Rais Kikwete hafahamu kuwepo mipango hiyo.  Ni vyema Mheshimiwa Lipumba aisaidie jamii kusema nani anafanya mpango huo ili ukweli ujulikane.  Aidha, Mheshimiwa Rais anawasihi wanasiasa na Watanzania kwa ujumla kuacha tabia za uongo na uzushi na kuwapotezea muda Watanzania kufikiria mambo yasiyokuwepo.
Ukweli ni kwamba, kama ambavyo amesema mara nyingi, ni matarajio ya Rais Kikwete kuwa mchakato wa Katiba utakamilika mwaka 2014 na kuwezesha Uchaguzi Mkuu wa 2015 kufanyika chini ya Katiba Mpya kama inavyotarajiwa na kumpa nafasi ya kustaafu mwisho wa kipindi chake cha uongozi wa taifa letu. 
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
15 Mei, 2013

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 16, 2013

    Michuzi, since you have direct or close relationship with his excellency interms of news dissemination, kindly advice for 'kurugenzi ya mawasiliano' information dissemination brush up, this kanusho, lile kanusho la dr slaa na matamshi mengi kutoka Ikulu yamekaa kimipasho, yakikosa weledi na kupunguza hadhi ya mheshimiwa Rais wetu, ni vizuri wafanyakazi wa serikali, hususani mahusiano na mawasiliano, wakitoa tamko kwa niaba ya mheshimiwa Rais wajiepushe kutoa matamshi yanayoonyesha chuki na mkanganyiko, au cheap propaganda za kupondana, pengine, Mheshimiwa Rais ampeleke huyu Salva kwa mwandishi wa hotuba za Rais wa Kenya, a 22year old, and a very bright and articulate young girl, pamoja na dominance kubwa sana ya CORD, hadhubutu kujibu kwa kuviponda bali kwa hekima na kuonyesha ukweli ulipo, ni hayo tu, maana wasaidizi wa mheshimiwa wasifanye wananchi wakajenga chuki na taasisi hii muhimu kwa Taifa letu. natumaini ujumbe umekufikia
    ni mimi mpenda maendeleo , mjenga nchi ninayeunga mkoni jitihada za mheshimiwa Rais wetu.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 16, 2013

    Your message was stellar, well constructed only came short as far as I'm concerned when you said we ni mpenda maendeleo and you r a due supporter of the present, wow, if u like maendeleo you wouldn't support the dude

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...