Januari 24, 2005: Ankal akiwa katika benchi la Serengeti Boys katika uwanja wa Barbourfields jijini  Bulawayo, Zimbabwe, wakati wa mpambano wa timu hiyo na timu ya Taifa ya Zimbabwe ya wachezaji walio chini ya umri wa miaka 17 chini ya kocha Abdallah 'King' Kibaden (wa pili kulia). 
Chini Serengeti Boys wakipiga jalamba kabla ya mchezo huo ambao vijana hao wa Tanzania walishinda kwa bao 1-0 na kufanikiwa kuvuka kuingia fainali ya kombe la Vijana wa Afrika zilizofanyika nchini Gambia. 
Bao la ushindi lilifungwa na Nizar Khalfani dakika ya 36 na kuwapa ushindi wa mabao 4-1 kufuatia mechi yao ya awali wiki mbili zilizopita uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam waliyoshinda bao 3-1

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 15, 2013

    ungetutajia majina hata ya wao walio katika benchi manake wengi sasa wamekuwa watu wazima

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 15, 2013

    Michuzi nisaidie ni vipi mwanangu ajiunge na hiyo timu kila siku tunafukuzana kwenye viwanja vya mchangani ili arudi kujisomea, yuko darasa la 7 na ana mpira mzuri.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 15, 2013

    Ankali ulikuwa huna kitambi kabisa ha, yani mika 8 tu umekuwa tofauti , atai , kitambi noma bwana

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...