Mkurugenzi wa Shirika la Kazi Kanda ya Afrika Mashariki nchini Tanzania (ILO) Bw. Alexio Musindo akikagua kinywaji aina ya ‘paw paw wine’ na mkononi akiwa ameshika matunda aina ya ‘rozela’ yanayotumika kwa kutengenezea ‘juice’ wakati alilipotembelea kikundi cha Chimbuko kinachoundwa na watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI Mjini Kyela mnamo tarehe 2, Aprili 2013 ili kujua maendeleo yao. Kikundi cha Chimbuko ni moja kati ya vikundi vya kijamii vinanvyonufaika na mradi wa UKIMWI kwa njia ya uwezeshaji Kiuchumi unaoratibiwa na ILO katika maeneo ipitayo njia kuu ya Tanzania – Zambia. (yaani Chalinze, Ilula, Mafinga, Makambako, Kyela na Tunduma).
Kwa habari na picha zaidi BOFYA HAPA


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 15, 2013

    leo ankali umechemsha ukurasa mzima wa blog ya jamii una habari mbili tu tena sio habari ni mapicha teh teh teh teh

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 15, 2013

    We baba una lako jambo, unasema ankal ana habari mbili tu? una makengeza? Acheni vijiba vya roho, vitawauwa! Nimefungua blog kama kumi za Bongo hadi sasa ni ankal pekee ana-update. Tena si habari za udaku kama unavyotaka wewe. Habari za jamii na maendeleo ambazo huzipati popote pengine. Ankal piga mzigo kaka, achana nao hao. Usikute huyo ana kiblogu kake kimemdodea anataka kutafuta sifa mgongoni kwako. Pole weeee...

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...