-Fomu za
wagombea zitaanza kuuzwa tarehe
2/5/2013 saa 2 asubuhi na mwisho w a
fomu hizo kuuzwa itakuwa tarehe 15/5/2013 saa kumi jioni.
-Fomu hizi
zitapatikana BMT, TAVA na kwa Makatibu wote wa vyama vya mikoa,
-Wagombea wa
nafasi za Mwenyekiti ,Makamu wenyeviti, Katibu mkuu na Katibu mkuu msaidizi
fomu zao zitauzwa kwa shilingi laki moja
na nusu (150,000)
-Wagombea wa
nafasi 8 za wajumbe watanunua fomu kwa
shilingi laki moja (100,000)
-Mgombea
atalipia ada ya fomu ya nafasi anayoitaka EXIM BANK, TANZANIA VOLLEYBALL
ASSOCIATION ACC. NO.0301381117.
-Mgombea
atapewa Bank slip ambayo ataiwasilisha na kupewa fomu, atayoijaza na
baadaye kuiscan pamoja na bank slip na kuituma TAVA- E mail
tavatanzania@yahoo. Com kabla au tarehe 15/5/2013 saa kumi jioni
-Siku ya Usaili
wa wagombea itakuwa tarehe 16/5/2013 kuanzia saa 4 asubuhi Katika hoteli ya
Mkonge jijini Tanga.
-Tarehe
17/5/2013 Kuanzia saa 2 asubuhi mpaka saa 12 jioni wagombea wataendelea na kampeni zao.
2.Sifa za wagombea
-Maombi ya
mgombea yapitishwe na chama cha mpira
wavu cha mkoa kilicho mwanachama wa TAVA
-Mgombea awe
anaweza kuandika na kuongea kingereza na Kiswahili
-Mgombea wa
mara ya kwanza asiwe chini ya umri wa miaka 30 na zaidi ya umri wa miaka 60
-Awe na
elimu angalau ya kidato cha nne.
-Awe ni mtu
maarufu katika familia ya mpira wa wavu
-Awe na
uwezo wa kutekeleza majukumu na shuguli za TAVA
-Kwa nafasi
ya Mwenyekiti, Makamu wenyeviti ,Katibu mkuu na katibu mkuu msaidizi mgombea
awe amewahi kuwa mjumbe wa bodi ya TAVA angalau kwa kipindi kimoja.
-Mgombea awe
na muda wa kutosha kutekeleza majukumu ya TAVA , angalau siku 30 kwa mwaka
katika nyakati tofauti.
Mgombea
asiwe amewahi kusimamishwa au kufukuzwa na TAVA, Chama cha mkoa , chama
chochote kingine cha michezo au shirikisho lolote la mchezo la kimataifa.
3.Mkutano mkuu wa uchaguzi.
-Tarehe 17/5/2013 saa 12 jioni Wajumbe wa mkutano
mkuu kuwasili jijini Tanga
-Tarehe 18/5/2013 saa 3 asubuhi mkutano kufunguliwa
rasimi.
-Tarehe 19/5/2013 Wajumbe kuondoka kuelekea makwao.
4. Gharama
za mkutano
-TAVA
Itagharimia chakula cha mchana kwa wajumbe wote tarehe 18/5/2013 siku ya mkutano.
Chama
cha mkoa kiwalipie wajumbe wake malazi,
na nauli zao za kwenda na kurudi.
.
Taarifa hii imetolewa na Mwenyekiti wa TAVA.
Augustino
Israel AGAPA



Kwanini Taarifa itolewe na Mwenyekiti na sio katibu wa chama? Na kwanini kila uchaguzi ni lazima ufanyikie Tanga tu,? Je Michuzi unaweza kumtafuta John Zambetakia mahala alipo ili tumshawishi agombee uongozi. tutamlipia gharama za fomu.
ReplyDelete