Heshima yako Ankal!!
       Nimepitia Blog yetu ya Jamii nikapata taarifa kuwa upo Singapore!! Yaani upo karibu kabisa nasi!! Sisi tupo Macau. Ni  Watanzania 12  ambao tunafanya kazi hapa katika Casino kubwa sanaaa na show tunayofanya ni kubwa sanaaa!! Jumanne na Jumatano ni Mapumziko!!

  Ombi langu nataka uje ututembelee Ankal. Ningependa kujua utaratibu wako niaje? Hata kama si mwezi huu hata kipindi kijacho,  maana huwa tunasikia tu viomgozi wetu na wadau kibao  wapo China ama Singapore kama hivyo, lakini hatujui jinsi ya kuwasiliana nao!! 

Tunatamani Serikali na Watanzania wenzetu wajue jinsi tunavyoitangaza Tanzania yetu Kimataifa hapa MAcau.   Maana ni Bahati sana kuwa katika show kubwa kama hii!!
Naandika kwa niaba ya Watanzania wenzangu tunaofanya kazi Macau katika show ya www.thehouseofdancingwater.com  iliyopo ndani ya City of Dream Casino, Macau

Nduguyo
Wabogojo
NB: Nakupa zawadi ya ngoma yangu hii uburudike na wadau


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 04, 2013

    Kipaji kipo!
    Nawatakieni kila la kher.

    Ila kumbukeni kuwekeza nyumbani maana kazi hizi umri ukienda ,sijui!!!!!!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 04, 2013

    Wabongo 'kwanza'nakupeni 5 kwa kuionesha tanzania popote tulipo!! hongera washikaji..

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 05, 2013

    huyu jamaa kama angeandaliwa mapema angetupatia medali kibao za olimpiki kwenye mambo ya sarakasi

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...