Salaam Ankal
Kwa kweli wajumbe wa tume ya katiba wameyatendea haki maoni ya watanzania juu ya katiba mpya. Ingawa sijapata muda wa kusoma kifungu hata kifungu kwa utulivu, lakini kwa muonekano wa awali rasimu ni nzuri na itahitaji marekebisho machache ya kimsingi.
Rasimu ya katiba imependekeza kuwepo kwa serikali tatu, yaani ya Muungano, ya Tanzania zanzibar(ambayo ipo kwa sasa) na ya Tanzania Bara( ambayo katika katiba ya zamani imo ndani ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania). Kwa utaratibu wa tume rasimu ya katiba itajadiliwa katika mabaraza mbalimbali yalioundwa katika ngazi tofauti na baadae kwenye bunge la katiba na mwishowe itapigiwa kura ya maoni na itakuwa tayari mwaka 2014. Serikali , inataka katiba hii ianze kutumika katika uchaguzi wa mwaka 2015.
Angalizo langu:
Iwapo katiba hii itapita katika mchakato mzima na ikakubalika kwa wananchi kwamba tuwe na serikali tatu. Serikali ya Muungano itakuwa na katiba, Serikali ya Tanzania Zanzibar wanayo katiba yao, Serikaliya Tanzania bara itakuwa haina katiba yake, hivyo basi tutabidi tuanze mchakato mpya wa kupata katiba ya serikali ya Tanzania bara mwaka 2014. Hili linaweza kuchukua muda mrefu na pengine kuchelewesha au kuhairisha uchaguzi wa mwaka 2015.
Sijui serikali na wanasiasa wanaliangaliaje hili.
Wadau wa blog je mna mawazo gani kuhusu angalizo hili?
Mambo ya muungano yatapunguzwa, yani liwepo la ulinzi tu. Litashughulikia masuala ya vifaa vya ulinzi tu. Raisi wa muungano ndiyo atakuwa na jukumu lake hilo. Ni zito sana. Lakini ukiangalia kwa juu juu utaona ni hakuna kitu.
ReplyDeleteMawaziri wa ulinzi wa tanganyika na zanzibar watahusishwa na raisi wa muungano.
Jina la muungano ni: Jamhuri ya Muungano wa Zanzibar na Tanganyika (United Republics of Zanzibar and Tanganyika).
Rasimu ya katiba iliyopo iendelee kuboreshwa kwa ajili ya Tanganyika. Kule Zanzibar nako waboreshe katiba yao kwa kipindi hichi hichi wakati mchakato unaendelea.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Zanzibar na Tanganyika itakuwa na maelezo ya mwanzo hayo na bunge lake, mahakama yake, na wafanyakazi wake.
Kila la kheri, tutengeneze kitu kizuri kwa vizazi vijavyo. Tutumie akili sana; tusiwe na jaziba.
kwanza nikuweke sawa mdau kuwa hakuna serikali itakayoitwa Tanzania Zanzibar what is tanzania zanzibar?
ReplyDeletekunatuwa na serikali ya Tanganyika, serikali ta Zanzibar na serikali ya Muungano wa tanganyika na zanzibar
lakini nchi itakayopewa jina la tanzania zanzibar?
jambo la pili labda hujailewa vizuri hiyo RASIMU rasimu imeweka kila kitu wazi kuwa kutakuwa na katiba ya Zanzibar ambayo ipo tokea awali kutakuwa na Katiba ya Tanganyika ambayo ipo tokea awali..
kuhusu katiba ya Muungano hakutokuwepo na katiba ya muungano badala yake kutakuwepo na SHERIA ya muungano
Sheria ya muungano wataachiwa wahusika wa mambo ya sheria wao ndio watakaotoa sheria hiyo
kwa maana wakiweka katiba kwenye muungano ina maana siku yoyote muungano ukiwa na tatizo itabidi katika ya muungano itolewe na ikitolewa ina maana itabidi kupoteza muda upya kwaajili ya kutengeneza katiba mpya
ili kusikuwepo na usumbufu wa kutafuta katiba mpya mara kwa mara ndio wakaona wasiweke katika kwenye serikali ya muungano waachiwe wana sheria waweke sheria ya muungano na sio katiba
nafikiri mpaka hapo utakuwa umepata kuelewa japo kidogo kwa ufahamu wangu mimi juu ya hiyo rasimu iliyotolewa.
POLE NA KAZI MDAU. MIMI NAKUUNGA MKONO MIA KWA MIA, SUALA LA SERIKALI TATU LIKIPITA, INA MAANA KWAMBA SERIKALI MOJA ITAKOSA KATIBA, YAANI SERIKALI YA TANGANYIKA. KAZI BADO NI MBICHI KABSAA. IN MY OPINION
ReplyDeleteWanalijua hilo, na hiyo imewekwa kimkakati kusogeza japo miaka miwili
ReplyDeleteAnkal, mi naomba nimtoe wasiwasi mdau kwa angalizo lake kwani ukiliangalia swala hili kwa haraka haraka unaweza ukaliona hilo. Lakini kwa ufahamu wangu mdogo nilionao juu ya jambo hili ni kwamba katika hizo serikali 3, inaonekana kwamba uchaguzi tutakaoufanya mwaka 2015 ni uchaguzi wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano, hivyo suala la katiba ya Tanzania bara halitaadhiri mchakato wa uchaguzi kwani tutahitaji katiba ya Tanzania bara isimame kwanza ndipo tufanye uchaguzi wa serikali ya Tanzania bara kama ambavyo wamekuwa wakifanya ndg zetu wa Tanzania Zanzibar. Hivyo nionavyo mimi ni kwamba uchaguzi mkuu wa 2015 utaendelea kama kawaida, na baada ya uchaguzi huo tutaanza mchakato wa kupata katiba ya Tanzania bara na ifikapo mwaka 2020 (kutoakana na katiba itakavyosema) basi unapofanyika uchaguzi mkuu wa JMT basi na uchaguzi wa Tanzania Bara na ule wa Tanzania Zanzibar utakapofanyika......ni hayo tu, Asalaam Aleykum
ReplyDeletenaona wadau mnashindwa kumwelewa aliyetoa mada...
ReplyDeletehuwezi kuunda muungano wa nchi mbili au zaidi bila ya kuwa na nchi hizo mbili au zaidi.... kwa maana hiyo tanganyika na zanzibar inabidi ziwepo kwanza kwa utaratibu unaoeleweka ambao ni katiba zao kamili kabla ya kwenda kutengeneza muungano
huyo anayesema katiba ya tanganyika simwelewi ni ipi anamaanisha
pia kama mkisema hii rasimu ni kwa ajili ya katiba ya tanganyika...je wanzibar walikua wanafanya nini kwenye hiyo tume
kwa uelewe wangu hili swala la muungano limewakoroga sana wajumbe wa tume.... theoretical solution ni serikali moja ila realistically ni ngumu....viongozi waliopo wanaogopa tu muungano usiwafie mikononi mwao kwa hiyo wanajaribu kusukuma tu mbele hili tatizo litafutiwe jawabu na awamu zijazo
Karibu Tanganyika!
ReplyDeleteYote kwa Yote Tuienzi kauli ya Marehemu Baba wa Taifa Mwl JK Nyerere.
ReplyDeleteMtakapojitenga - kwasababu tu ya ujinga/ulevi wa madaraka.... Mkajiita sisi na wao wao!! Hamtabaki salama! Baaada ya hao wao kuondoka nyie mliobakia mtajikuta kuna waflani na waflani na hao si wamoja! Hapo ndiyo mtakumbuka mlimwaga mboga mkabaki na ugali!! Sssa kuula mkavu ndipo itakuwa kimbembe!! Chezea mwalimu weye!!