Mahmoud Ahmad,Arusha
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni,Freeman Mbowe na Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini,Godbless Lema wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani hapa ilikuweza kutoa ushahidi wa tukio la bomu lililotokea kwenye mkutano wa kampeni wa chama hicho.
Viongozi hao wanashikiliwa baada ya Mwenyekiti huyo kudai anawajuwa waliolipua bomu na wanao mkanda wa tukio zima la ulipuaji huo wa Bomu kwenye mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Udiwani ulikuwa ufanyike Juni 16 jijini hapa.
Akizungumza na wanahabari kwenye ofisi za Makao Makuu ya Jeshi la Polisi mkoani hapa jana,Kamishna wa Upelelezi wa Jeshi hilo,Paul Chagonja alisema kuwa jeshi hilo linawataka viongozi hao waweze kuwasilisha ushahidi huo na kuwa kama hawatakubali kwa hiyari basi litawatafuta popote walipo.
Kamishna Chagonja alisema kuwa ushahidi wa tukio hilo ni muhimu kwa amani ya nchi yetu na kuwa machafuko yanayotokea kwenye jiji hili hayakubaliki kwani nchi yeyote iliyoingia kwenye machafuko ilichangiwa na vyombo vya habari kuripoti kwa ushabiki badala ya kutumia taaluma.

“Matukio ya ulipuaji wa mabomu kwenye nchi yetu hayakubaliki na kuwa mtu mwenye ushahidi wa tukio la bomu kwenye mkutano wa chadema atusaidie kuweza kufanya upelelezi wa tukio hili nawaombeni wanahabari kuacha ushabiki na kujikita katika taaluma yenu”alisema Chagonja.
Wakati huo huo Mwili wa aliekuwa Katibu wa Kata ya Sokoni 1 wa Chama hicho,Marehemu Judith William Mushi imepelekwa kuzikwa kwenye kata hiyo kwa heshima zote za chama hicho wakiwemo wabunge mbali mbali wa chama hicho waliopo mkoani hapa baada ya mwenyekiti wao kuwataka kushiriki kwenye tukio hilo.
Baadhi ya wabunge wa chama hicho waliopo mkoani hapa kushiriki msiba huo ni pamoja na mch.Peter Msigwa,Joseph Mbilinyi,Theresia Pareso,Ezekie Wenje,John Mnyika,na viongozi mbali mbali wa chama hicho kutoka makao makuu na mikoa ya jirani.
Aidha baadhi ya wananchi waliongea na mwanahabari hii waliieleza kuwa tumekuwa tukitafuta vipaji vya riadha hapa nchini lakini kumbe wapo hadi wabunge wanaoweza kutuwakilisha vizuri nchi yetu na tukapata hadi medali akiwemo mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema.
“unajua ndugu mwandishi mabomu sio mchezo yalimfanya mbunge kutimua mbio hadi maeneo ya sanawari hapa vipaji vipo ila hatujaweka mkazo kwenye kutafuta vipaji “alisema Yusuph.
Msafara wa kuupeleka mwili wa katibu wa kata ya Sokon 1 ulipitia kwenye barabara za Sokoine kuelekea Esso hadi Pallotkwenye nyumba yake ya milele na kuhudhuriwa na wafuasi wa chama hicho wengi wakitembea kwa miguu umbali wa kilometa sita kutoka Hospital ya mkoa ya Mout Meru.
Kweli utu watu umewatoka hata kwenye misiba wanaleta utani
ReplyDeleteThe Psychological Effects of Uniforms.
ReplyDeleteLook it up
Unajua last year niliona CNN Anderson cooper kwamba kiongozi yoyote anaevaa uniform tuu ni dictator .wakaanza majina ghafafi kuna Wakati nguo za jeshi kutwaa na nyota za kila aina hata Sadam Hussein ,North korea na jacket lake kutwaaaa,Mao wa china na suti Zake ata Nyerere alivaa sana hizo.Fimbo Nyerere fimbo na Mtu Mtu na fimbo .Anderson cooper Kwenye lile discussion waka conclude Politician are narcisstic
DeleteAngekufa mzaz au mwanae asingeleta mzaa wa haina hiyo,hayo ndiyo madhara ya kuvimbiwa makande .
ReplyDeletepoleni sana wafiwa. Mungu aiponye tz na watu wake.
ReplyDeleteDuh,chadema noma,wafuasi wake wapo kwa ajili ya kutukana,kukejeli viongozi na kutoa sifa zakijinga,sehemu zao kuu ni facebook,jamii forum na arusha..
ReplyDeleteThe real and lasting victories are those of peace, and not of war.
Ralph Waldo Emerson
Mbona Mbunge wa Kigoma Kabwe Zitto
ReplyDeleteHahuzulii Mazishi Arusha?? Na Vikao vingi haonekani?
Nyie wote hapo juu ni vilaza tu na hamjui mpo dunia gani! wapuuzi kama wazazi wenu
ReplyDeleteAstaghfir Allah
ReplyDeleteEwe Mnyalu wafikiri watu wote na wazazi wao wapuuzi,yaani hawana akili isipokuwa wewe. Umesema makubwa lakini nafikiri you are using the wrong mouth.Samahani kidhungu sitaki kuwakera waswahili.