Gari iliyobeba mwili wa Marehemu Albert Mangwea ikisukumwa na Mashabiki wake kutoka kwenye Sehemu ya maalum iliyokuwa imehifadhiwa maiti hiyo.Mwili wa Marehemu Mangwea umepelekwa kuhifadhiwa kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili,ambapo taratibu za kuuga mwili huo zitafanyika kesho kwenye Viwanja vya Leaders Club,Kinondoni jijini Dar kuanzia asubuhi.
Msafara ukielekea Muhimbili.
Gari maalum la Kubeba Mwili Msanii wa Muziki wa Kizaki Kipya,Marehemu Albert Mangwea likiwa tayari tayari kwa kubeba mwili.
Wadau mbali mbali wakiwa wamekusanyika kwa wingi kwenye uwanja wa Ndege Julius Nyerere kwa ajili ya kuupokea Mwili wa Marehemu Albert Mangwea uliowasili mchana huu kutokea nchini Afrika ya Kusini.
Wadau kibao wapo uwanja hapa hivi sasa tayari kwa kuupokea Mwili wa Marehemu Mangwea.
Rafiki kipenzi wa Marehemu Albert Mangwea,Jay Mo akihojiwa na vyombo vya hapari uwanjani hapa.
Prof. Jay nae alipata wasaha wa kuongea na vyombo vya habari juu ya Msanii mwenzao Albert Mangwea alietangulia Mbele ya haki.

KUONA PICHA ZAIDI

AU 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 04, 2013

    RIP Mangwea
    Tulikupenda lakini mungu kakupenda zaidi
    janetfashionandstyles.blogspot.com

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...