Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Bw. Laurence Bay, Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Singapore. Kushoto ni Balozi wa Tanzania India na Singapre Injinia John Kijazi na mbele yao ni Naibu Mkurugenzi wa Itifaki wa Singapore Bi. Christine Tay.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Mh. Bernard Membe,akifuatiwa na Waziri wa Viwanda na Biashara,Mh. Abdallah Kigoda pamoja na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Mh. Anne Tibaijuka wakati Rais akiwasili nchini Singapore leo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mbunge wa Kasulu mjini Mhe Moses Machali pamoja na wadau wengine wakati akiwasili Singapore.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea jijini Singapore leo wakati alipokutana na wafanyabaishara za ujenzi wa nchi hiyo marav tu baada ya kutua kutoka Japan alikokuweko kwa ziara ingine ya kikazi. Katika mkutano huu Rais Kikwete aliwakaribisha wafanyabishara hao wa Singapore Tanzania kuwekeza katika sekta ya nyumba wakati wa chakula cha jioni kilichiandaliwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).PICHA NA IKULU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 05, 2013

    Bongo tuna mengi ya kujifunza, mnaona hapo Rais anapokelewa na mkurugenzi, watu hufanya kazi na siyo kupoteza muda kupokea wageni. Bongo ingebidi magoma yote, mawziri wote etc kupokea mgeni.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...