Kwa katuni kedekede, tembelea jarida lako la katuni la mtandaoni, 'nathan cartoon magazine' kila Alhamis. Leo lipo angani kupitia chochoro hii,www.nathanmpangala.blogspot.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 20, 2013

    Vita Kimaslahi zaidi!

    Ni bora tungepeleka Majeshi Ziwa Nyasa kuikabili Malawi kwenye maslahi na sisi kuliko Kongo.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 20, 2013

    TZ wewe mtu mzima sasa!

    Kwa nini usinge jaribu kwa kuzaisha 'jiti' refu kupima kina cha maji hayo badala ya kwenda mwenyewe mzima mzima?

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 20, 2013

    Siri ya Vita isiyokwisha kule Mashariki ya Kongo wanaijua Jamhuri ya Rwanda!!!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 20, 2013

    TZ mjanja kweli kweli. Hajajirusha mzimamzima, kashusha miguu wakati mikono kashikilia. Akiona maji yanafika kwenye kitovu na bado hagusi chini atarudi haraka.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 20, 2013

    TZ jinsi alivyotanguliza tumbo mbele hawezi kurudi tena nyuma, kwani alivyoingia hivyo kutoka sio rahisi.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 20, 2013

    Kujaribu na maisha ya watoto zetu; mbona msiende wenyewe kutwa anga za burudani tuuuuu!

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 20, 2013

    Jamani tusiwe wasiopenda AMANI,Rais Jakaya Kikwete kasema ukweli... kuleta amani ndani ya great lakes region, Rwanda na Uganda waanze kwanza kuongea na wapinzani wao FDLR na LRA kama DRC inavyofanya na wapinzani wao M23...Nafkiri Watanzania tuunge mkono wazo hilo la Mtukufu Rais Jakaya Kikwete.
    Kuna wengi sana hawaelewi kwamba Tanzania ndio nchi inayokumbwa na janga hili la wakimbizi kutoka DRC,Burundi,Rwanda na Uganda.
    Jiulizeni kwa nini Rwanda na Uganda hawataki kukaa meza moja na wapinzani wao? jibu hizi ni tishio za Udikteta Afrika Mashariki na Kati.Jiulizeni kwa nini Rwanda ina makabila matatu tu(wahutu,Watutsi na Watwa) ila ya sioelewana? Tanzania ni nchi moja barani Afrika inayo heshimika kwa Amani na Demokrasia.Ndugu Anonymous "Vita Kimaslahi Zaidi" tusipendelee kupromoti vita na hatujui madhara yake...Tanzania imeombwa na Umoja wa Mataifa kupeleka majeshi Kongo sawasawa ungeliombwa kupeleka Darfour ao Syria na Afganistan.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 21, 2013

    Mdau wa 7 umenena,

    Ni muhimu Rwanda kukaa meza moja na FDLR na Congo kukaa meza moja na M-23 huku Uganda kukaa meza moja na ADF!

    Mhe. Raisi Kikwete amesema kweli kabisa na pia mwelekeo huo umeshuhudiwa na MAREKANI kufanya mazungumzo na TALIBAN !!! ni kitu ambacho huwezi kuamini Marekani wameona wakae na Taliban huko AFGHNISTANI ili amani irejee na vita isiyokwisha kusimama.

    Marekani ilianza kufanya maongezi hayo kwa siri huku Serikali wanayoilinda ya Afghanistani ya Hamid KARZAI ikiwa haijui lakini baadaye wakaja gundua kuwa maongezio kati ya AMERICA na TALIBAN yapo na juzi tu mpango wa AMANI umewekwa wazi.

    Sasa kama MAREKANI inaongea na TALIBAN(Magaidi) kusitisha vita na kuleta amani, je ni kosa gani alilofanya Mhe. Raisi Kikwete kumshauri Raisi Paul Kagame na Rwanda kufanya maongezi na FDLR?

    Ndio maana baada ya ushauri huo kwa kuwa Raisi Kagame ni mtu makini sana hakujibu kitu, ni kuwa ameridhia ushauri wa Mhe. Raisi Kikwete na kuwa amekubali kuwa ameelezwa ukweli!

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 21, 2013

    Hawa Rwanda nao wana makubwa!

    Ohhh Raisi Jakaya Kikwete na Tanzania yake ametudhalilisha kutushauri tuongee na Waasi wa FDLR!

    Dira ni kuleta amani ya kudumu sio mtu kudhalilika ama kudhalilishwa.

    Sasa kama Serikali ya Obama ya MAREKANI inaongea na TALIBAN kwa nini Rwanda na Kagame wasiongee na FDLR?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...