Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemhamisha Engineer Ibrahim Iyombe, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwenda kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi.
Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam leo, Alhamisi, Agosti 22, 2013 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue imesema kuwa Eng. Iyombe anachukua nafasi ya Engineer John Stanslaus Ndunguru ambaye atapangiwa kazi nyingine.
Aidha, taarifa imesema kuwa uhamisho huo unaanza mara moja.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.

Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Hongera sana Eng.Iyombe tunafahamu we ni jembe letu,mutu wa watu nenda ukafanye yako pale ujenzi!

    ReplyDelete
  2. Iyombe ni jembe c mchezo.all the best

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...