Meneja Chapa wa Tigo Bw. William Mpinga (kulia) akimkabidhi ufunguo wa Bajaji mshindi wa droo ya tatu wa promosheni ya Tigo ‘Miliki Biashara Yako’ Bw. Khalid Shabani katika hafla iliyofanyika Soko la Nyuki, Tegeta jijini Dar es Salaam.
Washindi wa droo ya tatu wa promosheni ya Tigo ‘Miliki Biashara Yako’ (kutoka kushoto) Bw. Sande Juma, Tito Mkude na Iddi Zonki wakikagua Bajaji walizokabidhiwa kutoka kwa kampuni hiyo ya simu katika hafla iliyofanyika Soko la Nyuki, Tegeta jijini Dar es Salaam.
Meneja Chapa wa Tigo, Bw. William Mpinga akihojiwa na Waandishi wa Habari katika hafla ya makabidhiano ya washindi wa promosheni 'Miliki Biashara Yako' iliyofanyika Soko la Nyuki, Tegeta jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...