Wakala wa Majengo (TBA), ulianzishwa mwaka 2002 kupitia Sheria ya Wakala Namba 30 ya mwaka 1997. Lengo la kuanzishwa TBA ni kutoa huduma bora na ya gharama nafuu ya makazi kwa watumishi wa umma na ofisi kwa Serikali na Taasisi zake.

Ikiwa ni taasisi muhumu ya Serikali iliyochini ya Wizara ya Ujenzi, TBA imeshiriki maonesho ya Wakulima maarufu Nane Nane ambayo hii leo yanafikia Kilele katika kanda mbalimbali na Kitaifa yanafikia Kilele katika Viwanja vya Nzuguni, mjini Dodoma.

Timu ya TBA iliyo katika banda lao Viwanja vya Nzuguni jana ilitembelewa na Blog hii na kuikuta ikiwa kamili katika utoaji huduma kwa wananchi ya nini ambacho TBA inakifanya kila siku katika utekelezaji wa shughuli zake.

Timu hiyo pichani kutoka kushoto ni Kaimu Afisa Uhusiano, Mariam Lusewa, Meneja Miradi Maalum, Edwin Nnunduma, Afisa Miliki, Pendaeli Mhufu na Mhandizi Mazingira, Mtapuli Juma.
 Afisa Miliki, Pendaeli Mhufu (kushoto) akihudumia wananchi.
 Wageni wakisaini kitabu cha kutembelea banda hilo na kutoa maoni yao juu ya huduma.
 Kutoka Kulia ni Pendaeli Mhufu, Mariam Lusewa na Mtapuli Juma wakiwa na nyuso za furaha wakati wa kuhudumia wananchi waliotembelea banda lao Nzuguni Dodoma.
 Kaimu Afisa Uhusiano, Mariam Lusewa akiwasikiliza mwananchi  aliyetembelea banda lao jana kupata taarifa mbalimbali.
 Meneja Miradi Maalum, Edwin Nnunduma pamoja na Kaimu Afisa Uhusiano, Mariamu Lusewa wakiwasikiliza wananchi na kuwapa maelezo ama majibu ya maswali yao.
Kaimu Afisa Uhusiano, Mariam Lusewa akimsikiliza mwananchi aliyetembelea banda lao jana kupata taarifa mbalimbali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...