Mshambuliaji wa Uruguay Luis Suarez akishangilia leo baada ya kurudi kwa kishindo kwenye ligi Kuu ya Uingereza baada ya kupiga mabao mawili wakati Bwawa la Maini likiipiga Sunderland bao 3-1 na kuruka hadi nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo.
Akicheza kwa mara ya kwanza toka April 21 kutokana na kufungiwa michezo 10 kwa kumng’ata mtu, Suarez aliona nyavu mara mbili baada ya kutengenezewa na Daniel Sturridge, ambaye alifunga bao la kwanza akiwa ndani ya sita.
Emanuele Giaccherini alirudisha moja lakini Bwawa la maini waligangamara, na endapo kama Liva ingeshinda 2-1 wangebaki katika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi, lakini bao la tatu la Suarez limewanyanyua.
Suarez alirejea rasmi wiki iliyopita wakati Bwawa la Maini lilipokipiga na Man U na kufungwa kwa bahati mbaya bao 1-0, ila mchezo wa leo ulikuwa wa kwanza kwake na kaonesha yeye na Sturridge ni ‘mapacha’ wenye sumu kali uwanjani.
CHEKI MSIMAMO HADI SASA.
MAN U MLIE TU MWAKA HUU...
CHEKI MSIMAMO HADI SASA.
MAN U MLIE TU MWAKA HUU...
1 | Arsenal | 6 | 6 | 15 |
2 | Liverpool | 6 | 4 | 13 |
3 | Tottenham | 6 | 4 | 13 |
4 | Chelsea | 6 | 4 | 11 |
5 | Southampton | 6 | 3 | 11 |
6 | Man City | 6 | 7 | 10 |
7 | Hull | 6 | -1 | 10 |
8 | Everton | 5 | 2 | 9 |
9 | Aston Villa | 6 | 1 | 9 |
10 | West Brom | 6 | 1 | 8 |
11 | Cardiff | 6 | -1 | 8 |
12 | Man Utd | 6 | 0 | 7 |
13 | Swansea | 6 | -1 | 7 |
14 | Norwich | 6 | -2 | 7 |
15 | Stoke | 6 | -2 | 7 |
16 | Newcastle | 5 | -3 | 7 |
17 | West Ham | 6 | -1 | 5 |
18 | Fulham | 6 | -5 | 4 |
19 | Crystal Palace | 6 | -6 | 3 |
20 | Sunderland | 6 | -10 | 1 |
Mh! Hili bwawa lako la maini naona kama ni bidhaa ya kichina, urembo mwanzo tu, wenye shughuli yao wanakuja, hawana haraka.
ReplyDeleteTable hiyo tuwekee ikifika January, nina hakika hutaiweka!!
ReplyDeleteJamaa ndugu zangu mashabiki wa Manu siku hizi wamepoteza kauli, wakiniona tu watafuta sababu za kuondoka ati wana mashughuli. Nawaonea huruma.Ila huyo kocha mpya mwambie atafute kazi nionavyo mimi akipoteza mechi mbili hivi zaidi, atanyolewa manyoya ya shingo.
ReplyDelete