Bondia wa ngumi za kulipwa nchini Karama Nyilawila (pichani) alishawahi kuubeba ubingwa wa dunia wa  WBF –middle weight  kwa kumpiga Kreshnik Qato wa Czech Republic, katika ukumbi wa Sparta arena, Plaque.

Ubingwa  huo ambao una hadhi kama aliokuwa nao Francis Cheka kwa sasa, baadae aliupoteza kwa kutoutetea kutokana na kukosa wadhamini wa kumsaidia kuutetea ubingwa wake huo, na kushawishika kucheza na Francis Cheka  katika pambano alilopoteza na kukaa kimya muda mrefu bila kucheza  pambano la ndani ya nchi.


Karama anategemea kupanda ulingoni  tena tarehe 20 ya mwezi wa kumi katika ukumbi wa ccm mwinjuma.Mwananyamala  kuzipiga na sado philemon katika pambano lililoandaliwa na  Bigright promotion.
Akilizungumzia pambano hilo Ibrahim kamwe anaeleza kuwa maandalizi mpaka sasa yanaenda vizuri pindi yapo katika mazingira magumu kwa wale watakaocheza utangulizi wanajiandaa kiukataukata kwa ajili ya pambano hilo ambalo litakuwa na mapambano mengi ya utangulizi, ukizingatia hatujapata mdhamini wa kudhamini pambano hili ili liwe katika ubora unaotakiwa , lakini tunapambana na tutajitahidi  pambano lifanyike vema tuwatie moyo hawa mabondia wanaochipukia na kuusimamisha vizuri mchezo wetu wa masumbwi.
Karama na mwenzie Philemon wameshasaini makubaliano ya mchezo huo na wapo katika hali nzuri ya kimchezo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...