Mkongwe wa muziki wa kizaz kipya a.k.a Bongofleva Afande Sele a.k.a Baba Tunda a.k.a Simba Mzee akidhihirisha ukongwe juu ya steji ya tamasha la Serengeti linalofanyika usiku huu ndani ya uwanja wa Jamuhuri mkoani Dodoma,ambapo maelfu ya watu washabiki wamejitokeza kushuhudia tamasha hilo ambalo hufanyika mara moja kwa mwaka.
 Msanii mahiri ambaye kwa sasa anasumbua vilivyo anga ya muziki wa Bongofleva,Diamond akiwaimbisha mashabiki wake usiku huu kwenye tamasha la serengeti fiesta 2013,linalofanyika usiku huu kwenye uwanja wa Jamuhuri.
Haaaa haaaa...ukitaka kubana pua kabane nyumbani kwenu,hapa ni hip hop tuuu.....Msanii wa Bongofleva Ney wa Mitego wakioneshana umahiri umwamba wa jukwaani na msanii mwenzake  Dimond  kupitia wimbo wa Muziki Gani.
Maelfu ya Watu wakiwa kwenye uwanja wa jamuhuri,usiku huu wakishangweka na tamasha la Serengeti Fiesta 2013.
 Mwanadada ambaye wengi wanadai amerithi viuno na sauti kutoka mwanamuziki Ray C,anaitwa Rachael kutoka nyumba ya vipaji a.k.a THT akiimba jukwaani huku akionesha umahiri wake wa kukata mauno.
PICHA ZAIDI LIVE INGIA MICHUZIJR.BLOGSPOT.COM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...