Timu ya mpira wa Pete ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma imeendeleza ubabe katika mashindano ya SHIMIWI yanayoendela katika viwanja vya Chuo Kikuu Dodoma baada ya kuichakaza timu ya Mifugo kwa magoli 28 kwa 15 jana jioni.
Mchezo huo ulioanza kwa kasi huku kila timu ikimsoma mpinzani wake hata hivyo Mifugo ilipelekwa kasi na Utumishi kwa kukubali magoli 16 kwa 6 hadi kipindi cha kwanza kinamalizika. Katika kipindi cha kwanza Mifugo walipoteza pasi 10 kwa kudhibitiwa na Monica Aloyce (GK) na Amina Ahmed (WD) wa Utumishi.
Kipindi cha pili kwa kiasi kikubwa kilimilikiwa na Utumishi hali iliyowafanya wachezaji wa Mifugo kucheza ndivyo sivyo.
Mchezo wa rafu ulisababishwa mechi hiyo kusimamishwa mara kadhaa ambapo Fatma Ahmed (GS) na Secela Shabani (WA) wote wa Utumishi kuumizwa. Katika kipindi hicho Utumishi ilijiongezea magoli 12 na Mifugo kuambulia 9.
Baada ya mchezo huo Kocha wa timu ya Utumishi Bw. Mathew Kambona alisema mechi ilikua nzuri licha ya wachezaji wake kuumizwa kutokana na mchezo wa rafu.
“Tunajipanga vizuri ili kuhakikisha wachezaji walioumizwa wanakuwa sawa kwa michezo inayokuja” Kambona alisema.
Hata hivyo, kocha wa Mifugo Bi. Nora Nchuwekeleze alisema bado anaamini timu yake ni nzuri.
Nchukuwekeleze alisema mchezo ulikuwa mzuri na wenye wenye ushindani.
Mwanamkasi Abbasi (GK) anayeichezea Mifugo alisema walizidiwa kutokana na wachezaji watatu tegemeo kuwa majeruhi hivyo kuzidiwa mbinu na maarifa na wapinzani wetu.
Timu ya Utumishi itaingia katika mzunguko wa pili wa Michezo ya SHIMIWI kwa upande wa mpira wa Pete baada ya kupatikana kwa mshindi katika mchezo kati ya Wizara ya Viwanda na Biashara na Wizara ya Katiba na Sheria mechi itakayochezwa leo jioni.
Timu ya mpira wa pete ya Utumishi kabla ya kuanza kwa mechi kati yake na Wizara ya Mifugo katika viwanja vya UDOM mjini Dodoma.
Timu ya Wizara ya Mifugo kabla ya kuanza mechi kati yake na timu ta Utumishi katika viwanja vya UDOM mjini Dodoma.
Timu ya mpira wa pete ya Utumishi ikisalimiana na timu ya Mifugo kabla ya mechi kuanza katika viwanja vya UDOM.
Timu ya Utumishi ikimenyana na timu ya Mifugo katika viwanja vya UDOM mjini Dodoma
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...