Madubi Marcely afisa Mradi wa kuboresha uzalishaji na upatikanaji wa masoko kwa mazao ya horticulture-Morogoro kutoka iWASH akinena na washiriki wa Warsha hiyo. Kushoto ni Isaac Ndamanhyilu Mtaalamu wa masuala ya kilimo cha mazao ya Horticulture kutoka TAHA na kulia ni George Mhina Afisa kilimo na mifugo wa wilaya ya Mvomero, Morogoro.
Washiriki wakimsikiliza Ndugu Isaac Ndamanhyilu wakati wa Warsha hiyo.
Anani Bansimbile Afisa mradi wa kuboresha uzalishaji na upatikanaji wa masoko kwa mazao ya horticulture-Morogoro kutoka TAHA-Morogoro akichagiza neno wakati wa mjadala kwenye Warsha iliyofanyika ukumbi wa Gwami Executive Hotel, Morogoro.
Washiriki wa Warsha wakiwa ukimbini
Bi. Cyrila Mlay, Afisa masoko kutoka TAHA akizungumzia juu umuhimu wa masuala ya uzalishaji wa mazao ya horticulture kwa kuzingatia mahitaji ya Masoko.

Mandhari ya Mji wa Morogoro eneo la Msamvu ambapo Warsha inafanyika
Tanzania Horticultural Association (TAHA) yenye makao makuu yake Arusha na ofisi ndogo Mkoa wa Morogoro leo imefanya Warsha ambayo imelenga Kuwaleta pamoja Wadau wa mazao ya horticulture hasa Wakulima (Wazalishaji) na Wanunuzi (Soko) ili kuainisha changamoto zinazowakabili na hatimaye kuwaunganisha pamoja ili waweze kufanya biashara pamoja.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...