Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa, akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa duka la huduma kwa wateja la Vodacom lililoko Msimbazi kariakoo jijini Dar es Salaam. Pamoja nae katika picha ni Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania, Hassan Saleh kulia na Mkurugenzi wa Planetell David Hayes. Hilo ni duka la 70 la kampuni hiyo nchini.
Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania, Hassan Saleh, akimfafanulia jambo Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa kuhusu mfumo wa uhifadhi wa taarifa za M-pesa zinazowahusu wateja wakati Meya akiangalia huduma mbalimbali zinazotolewa kwenye duka jipya la Vodacom Msimbazi mara baada ya kulizindua.Wengine pichani ni Meneja wa duka hilo Josephine Swai na Mkuu wa kitengo cha Mauzo wa Vodacom .
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa (kulia), akisalimiana na Mkurugenzi wa Pantell David Hayes wakati akiwasili kwa ajili ya ufunguzi wa Duka jipya la Vodacom lililoko Msimbazi kariakoo jijini Dar es Salaam, Wanaoshuhudia wa kwanza kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Mauzo wa kampuni hiyo Upendo Richard, Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania, Hassan Saleh na Meneja uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim.
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mfanyakazi wa wa duka jipya la Vodacom Msimbazi namna huduma zinavyotolewa kwa wateja wa kampuni hiyo. Wa kwanza kulia ni Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania, Hassan Saleh. Meya Silaa alilizundua rasmi duka hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...