Mkurugenzi wa Huduma kwa Wanachama wa LAPF, Valerian Mablangeti, akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu Mkutano wa Sita wa Wadau wa LAPF utakaofanyika Arusha siku ya Ijumaa na Jumamosi. Kushoto ni

Meneja wa LAPF, Kanda ya Mashariki, Amina Kassim na Kulia ni Meneja Matekelezo wa LAPF, Victor Kikoti.
 Mkutano ukiendelea
 Wanahabari wa Arusha wakiwa makini kazini
Mtayarishaji mashuhuri wa vipindi vya kimaendeleo katika Luninga Bw. Pascal Mayala akiwahoji viongozi wa LAPF katika mkutano huo 
-------------------------------------------
Mfuko wa Pensheni wa LAPF unatarajia kufanya mkutano mkuu wa sita wa Wadau wake tarehe 11- 12 Oktoba 2013 katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa AICC Jijini Arusha.
Kauli mbiu ya mkutano huoni  “ KUKIDHI KWA MAFAO YA KUSTAAFU; CHANGAMOTO NA NJIA ZA KUBORESHA.” Kauli mbiu hii imefikiwa baada ya kuwepo kwa hoja zinazojadiliwa mara kadhaa kwamba mafao ya pensheni yanayolipwa kwa wastaafu hayakidhi. Wadau wa mkutano huu watajadili kwa kina juu ya Kauli mbiu hii na kuona kama je  ni kweli mafao yanayotolewa yanakidhi changamoto za uzee ama ni kutokana na maandalizi hafifu  ya kustaafu.
Mkutano huu utafunguliwa na Waziri wa nchi katika ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe: Hawa Ghasia
Washiriki wa mkutano huu ni pamoja na Mamlaka ya Hifadhi ya Jamii, Waajiri wachangiaji, wanachama, vyama vya wafanyakazi, taasisi mbalimbai za umma na binafsi pamoja na Mifuko ya Hifadhi  ya Jamii ya ndani na nje ya nchi.
Waajiri wachangiaji wa LAPF kwa sasa wanatoka katika makundi yafuatayo:-
·         Halmashauri zote za majiji,Manispaa, miji na wilaya nchini.
·         Wizara zote za serikali
·         Taasisi zote za serikali
·         Mashirika ya umma
·         Sekta binafsi
·         Mashirika yasiyokuwa ya serikali (NGO’s), Wajasiriamali.
Mada mbalimbali zitawasilishwa kutoka ndani na nje ya Tanzania zikijadili kauli mbiu hyo ambazo ni pamoja na:
·         Mada anzilishi juu ya kauli mbiu ya mkutano.
·         Mada juu ya dhana ya kukidhi kwa mafao ya kustaafu.
·         Mada ya ulinganifu wa mafao kwa nchi mbalimbali za Afrika mashariki na kati.
·         Mada ya ujasiriamali.
·         Mada juu ya taarifa za utendaji wa Mfuko kwa mwaka wa fedha ulioshia Juni  2013 pia zitajadiliwa
LAPF imekuwa ikifanya mikutano hii Kubadilishana mawazo na wadau wake na kupata maoni mbali mbali jinsi ya kuroresha huduma zinazotolewa kwa manufaa ya wanachama wake.
Kwa sasa  Mfuko unatoa mafao mbalimbali kama :
·         Mafao ya uzeeni (old age pension benefit)
·         Mafao ya Mirathi ( survivorship benefit)
·         Mafao ya Kuumia kazini (invalidity benefit)
·         Mafao ya kujitoa (withdrawal benefit)
·         Mafao ya uzazi (maternity benefits)
·         Msaada wa mazishi (Funeral grants)
·         Mikopo ya nyumba (House loans)
·         Mikopo ya wanachama kupitia SACCOS
Waalikwa wote mnaombwa kuhudhuria bila kukosa katika mkutano huu muhimu.
STAAFU KWA UFAHARI NA LAPF.

Imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa LAPF.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...