Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Ramadhan Mwinyi akizungumza wakati wa  mkutano  uliokuwa ukijadili kuhusu  Maendeleo ya Jamii,  na mkazo mkubwa ukisisitizwa katika maendeleo endelevu yanayojumuisha makundi  yote  likiwamo kundi la Wazee. 
Akizungumzia  uzoefu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika  utekelezaji wa sera na mipango mbalimbali inayolenga kuwapatia unafuu wa maisha wazee, Balozi Mwinyi alieleza kwamba kwa kutambua mchango mkubwa wa kundi hilo la Jamii , Tanzania licha ya changamoto mbalimbali imejiweka sera na mipango inayojikita katika kutoa unafuu wa maisha kwa  wazee. 
Akazitaja  baadhi ya huduma hizo kuwa ni pamoja na huduma za afya na makazi kwa wazee wasiokuwa na uwezo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...