Wakazi wa Makete mjini wilayani Makete mkoani Njombe wameonesha mfano wa kuigwa na nchi nzima baada ya kutii agizo la serikali liliowataka kubomboa nyumba zilizopo kandokando mwa barabara ndani ya kipindi cha mwezi mmoja

Zoezi hili la kubomoa nyumba hizo lilitakiwa kufanywa ndani ya kipindi cha mwezi mmoja ili kupisha ujenzi wa barabara ya lami Makete mjini kama ilivyoahidiwa na serikali

Mtandao huu ulishuhudia zoezi la kubomoa nyumba hizo likitekelezwa kwa zaidi ya asilimia 95 huku wananchi hao wakiitaka serikali kuharakisha kujenga barabara hiyo kwa wakati kwa kuwa wameahidiwa kwa muda mrefu

"Sisi tunapenda maendeleo ya wilaya yetu ndio maana unaona tunabomoa bila usumbufu, lakini isiwe tunabomoa halafu ujenzi unakuja kuanza miaka ijayo huko mbele huu utakuwa ni uonevu wa hali ya juu kwa kweli" alisema mfanyabiashara mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la Chaula

Wabomoaji hao wameendelea kubomoa nyumba zao kwa umakini na kuchukua baadhi ya vifaa kama tofali, milango, madirisha na mbao ili waweze kwenda kuvitumia kwenye maeneo mengine waliyoyapata
Kwa mujibu wa tangazo la TANROADS mkoa wa Njombe, zoezi la kubomoa kwa hiari limemalizika na kwa yeyote ambaye hatakuwa ametii amri hiyo, bomoa bomoa ya serikali itapita ili kuondoa jengo hilo(na www.edwinmoshi.com)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Nadhani walilipwa kwa wakati muafaka na kupewa maeneo mapya kwa wakati muafaka.Iwapo maeneo yote yaliyopita na hata yaliyo ktk mipango kama hii kwa siku za usoni yatafanyiwa utaratibu huu naamini hutasikia mtu akilalama au kuleta usumbufu.Bila kusahau uongozi wa eneo husika kusimama imara kwa kuwajuza wananchi wa maeneo yao kila linaloendelea mpaka kufikia hatua ya kubomoa,vinginevyo lawama,au usumbufu hautaepukika.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...