Mwenyekiti  wa chama  cha  waandishi  wa habari mkoa  wa Iringa Frank Leonard kulia akitoa msimamo  wa  wanahabari dhidi ya  gazeti la Rai na mbunge Msigwa  leo ,kushoto ni katibu mtendaji wa IPC Francis Godwin
 Wanahabari Clement Sanga kushoto akiwa na mwakilishi  wa New habari {2006} Ltd  wachapishaji wa magazeti ya Mtanzania , Rai  na Bingwa mkoa  wa Iringa Mercy Mwalusamba wakati  wa kikao  cha  cha wanahabari  mkoa  wa Iringa  leo  kujadili habari  zilizoandikwa na gazeti la Rai Jumapili.

Na  Francis Godwin

WANAHABARI  mkoani Iringa wamekanusha  vikali habari  zilizoandika na gazeti la Rai  toleo namba 1067 la  jumapili wiki iliyopita kuwa wanahabari  mjini Iringa  wamehongwa fedha na  viongozi  wa CCM mkoa  wa Iringa ili  wasiandike habari ya msaidizi  wa mbunge Wiliam Lukuvi Bw Thom Malenga kukamatwa  kwa  tuhuma  za kujihusisha na ujangili.

Wahanabari  hao  katika  kikao  chao kilichofanyika   leo  katika  ofisi  za klabu ya  waandishi  wa habari mkoa  wa Iringa (IPC) mbali ya  kukanusha habari  hizo  kuwa zimeandikwa kwa  lengo la  kuchafua  tasnia ya habari mkoa  wa Iringa ila bado wanalitaka  gazeti  la Rai  na mbunge wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa  kuwataja  waandishi  waliohongwa na  viongozi  wa CCM mkoa  wa Iringa kabla ya  wanahabari  hao  hawajachukua  hatua zaidi  dhidi ya gazeti  la rai pamoja na mbunge Msigwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...