Naibu Katibu Mkuu wa Shirikisho la 
Michezo Wizarani Bw.Moshi Makuka 
Naibu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Michezo la Wizarani (SHIMIWI) Bw. Moshi Makuka amesema shirikisho hilo linatarajia kufanya mkutano wa tathmini wa mashindano ya SHIMIWI ya mwaka huu mjini Morogoro tarehe 13 na 14 Desemba, 2013.
Akiongea ofisini kwake Bw.Makuka alisema kuwa lengo kuu la mkutano huo ni kujadili changamoto zilzojitokeza kwenye mashindano ya mwaka huu.
“Lengo ni kujadili changamoto zilizojitokeza katika mashindano ya SHIMIWI ya mwaka huu na kuzipatia ufumbuzi kwa ajili ya kuboresha michezo ya mwaka ujao” alisema Bw.Makuka.
Aidha,Bw Makuka aliwataka Wenyeviti wa vilabu,Makatibu wa Vilabu na Maafisa Michezo kufika bila kukosa ili kukuza michezo serikalini.
“Wenyeviti,Makatibu na Maafisa Michezo wa vilabu wahudhurie kwa wingi ili waje kutoa changamoto zao walizokutana nazo katika michezo ya mwaka huu” alifafanua Bw.Makuka.
Shirikisho la Michezo Wizarani (SHIMIWI) kila mwaka huandaa michezo inayowakutanisha watumishi wa serikali kutoka katika Wizara,Idara zinazojitegemea,Wakala wa serikali na Ofisi za Wakuu wa Mikoa ambapo kwa mwaka huu yalifanyika mjini Dodoma kuanzia tarehe Septemba 21 hadi Oktoba 5.
Wajumbe wanaotakiwa kuhudhuria mkutano huo ni Mwenyekiti, Katibu na maafisa michezo wote kutoka vilabu vya SHIMIWI. Hadi sasa mikoa ya Dodoma na Kilimanjaro imeshatuma maombi ya kushiriki, na mikoa mingine inahimizwa kufanya hivyo mapema iwezekanavyo>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...