Na Abdulaziz Video, Lindi
Wananchi wa wa vijiji vya Singino wilayani Kilwa mkoani Lindi wamelalamikia Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira(NEMC )kwa kitendo cha kutokusimamia vyema kazi iliyopewa na Bodi ya Korosho Tanzania katika zoezi la uteketezaji kemikali zilizotelekezwa kwa zaidi ya miaka 20 zinazosadikika kuwa sumu inayoweza kuathiri afya ya binadamu, mifugo na mimea. 
Akizungumza kwa niaba ya wananchi hao Diwani wa kata ya Kivinje, Bw. Jafari Arobaini na Mwenyekiti wa kijiji cha Singino Maulidi Mbulula walisema kitendo cha mkandarasi kumwaga ovyo dawa hizo kunaweza kusababisha madhara makubwa kwa wananchi,mifugo na mimea na kuathiri kukua kwa mji huo. 
Pamoja na zoezi hilo kusimamiwa na watu wa mazingira lakini bado zoezi linaonyesha kutotekelezwa kama lilivyopangwa katika makubaliano ya pamoja kati ya serikali ya kijiji, halmashauri, na NEMC baada ya kukutwa kemikali hizo zikiwa zimemwagika njiani 
 Bw. Bakari Mussa Mkazi wa kilwa Masoko ambae alipata kazi katika ghala hilo alieleza athari alizoziona na kuacha kazi hiyo kulinda afya yake huku Abdu Saidi mjumbe wa Singino ameomba uongozi wa wilaya kusimamisha zoezi ili kunusuru maisha ya wananchi wa eneo hilo kutokana na ukiukwaji unaoonekana sasa kazi inavyoendelea. 
 Kwa upande wake Afisa msimamizi mazingira NEMC Jorome Kayombo alisema kuwa awali NEMC ilimwagiza mkandarasi kuchimba shimo futi tano na kutandika kapeti chini, pembeni na juu ili kuzuia mwingiliano wa kemikali hizo na udongo huku akikataa kupigwa picha na kutoa ufafunuzi zaidi wa kemikali hizo kwa madai si msemaji wa NEMC 
Katika hali isiyo ya kawaida Uongozi wa ghala hilo ulimwamuru mlinzi kutoruhusu waandishi kuingia kuangalia hali ya utoaji wa madawa hayo ghalani kufuatia malalamiko ya vibarua wanaofanya kazi hiyo hatarishi
Eneo la uteketezaji kemikali hizo
Mkaazi wa maeneo ya Singino wilayani Kilwa mkoani Lindi akionesha hali ilivyo
Mmoja wa mifuko ukiwa umeanguka chini

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...