Miongoni mwa vitendo vinavyoshamiri Makete vya watoto kujihusisha na biashara ya kuuza mkaa
 Mkaa ukisubiri wateja.
-------
Na Edwin Moshi,Makete.

Mafunzo ya ulinzi na usalama wa mtoto dhidi ya ukatili na unyanyasaji yaliyoanza jana wilayani Makete mkoani Njombe yanaendelea katika ukumbi wa Sumasesu Tandala

Mafunzo hayo yaliyofunguliwa na Afisa Ustawi wa Jamii wilaya ya Makete Bw. Leonce Panga yameshirikisha wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini, dawati la jinsia kutoka kituo cha polisi Makete, maafisa elimu, mwanasheria, magereza, wauguzi, madaktari pamoja na hakimu mfawidhi wa wilaya ya Makete

Katika mafunzo hayo yanayowezeshwa na Bi Asha Mbaruku pamoja na Ramadhani Yahaya kutoka  ustawi wa jamii makao makuu jijini Dar es Salaam wamesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wadau hao namna ya kuwahudumia watoto wanaokuwa wamefika kwenye ofisi zao kupata msaada endapo anakuwa amepata tatizo akitolea mfano kufukuzwa shule kwa kukosa ada

Wamesema washiriki hao wanapaswa kuwa timu ya ulinzi na usalama wa mtoto ili waweze kumsaidia mtoto, huku Bi Asha akisisitiza kuwa kuna huduma ya msaada kwa watoto wanaofanyiwa vitendo vya ukatili iliyoanzishwa wizarani inayoitwa huduma mtandao (Child helpline) inayohusu mtoto kupiga simu moja kwa moja na kueleza shida yake na kupatiwa suluhu

Washiriki pia wamefundishwa njia mbalimbali za ufundishaji wa masuala ya ulinzi na usalama wa mtoto kwa ngazi ya chini ya serikali

Kwa upande wao washiriki wametoa visa mbalimbali vinavyoendelea katika jamii ya Makete ikiwemo kata ya Mbalatse ambayo watoto wa kike wanafanyiwa vitendo vya ukeketaji kwa siri kubwa

Mafunzo hayo yameweka wazi hatua zinazochukuliwa na serikali kupambana na vitendo vya ukatili kwa watoto ikiwemo kutunga na kusimamia sheria mbalimbali zinazomlinda mtoto


Mafunzo hayo ya siku 5 yaliyoanza jana yameandaliwa na ustawi wa jamii makao makuu jijini Dar es Salaam na yanatarajiwa kuhitimishwa Jumamosi wiki hii

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Wanyalu Wilayani Makete.

    Ohhhh Sarafu mnaichungulia vibaya sana, watoto badala ya kuwapeleka Shule kusoma mnawakabidhi Mikaa kuuza?

    ReplyDelete
  2. Sasa wakale wapi? Wazazi wao wahahitaji msaada, wao wako shambani, watoto wanauza mkaa nyumbani. Msitake kuiga mambo ya ughaibuni. Wao wanawapa watoto "child benefit" na wazazi "unemployment benefit" kwa hivyo hakuna sababu ya watoto kunyanyaswa.

    ReplyDelete
  3. Ni matokeo ya ubinafsi wa viongozi.
    Kwani Tanzania inashindwa kuwa benefit kama za ulaya wakati nchi ina kila utajiri kutoka kwa mwenyezi mungu?
    Ni uroho wa utajiri kwa walio juu kushindwa kutatua haya matatizo ambayo si kweli kwamba nchi yetu haina uwezo kuyatatua.
    Tutabakia hivihivi mpaka mungu atuangamize au atutie majaribu makubwa, labda ndio tutakumbuka.

    ReplyDelete
  4. System ya nchi ipo corrupted,period!
    Ulaya na TZ kwa sasa ni sawa tu.Tuna wasomi,migodi ya madini, gas, wanyama, bandari,tunalipa kodi nk nk.
    Tuna taka nini tena tuweze kujikwamua ? Tatizo ni kuwa kila mradi kuna 10% ya watu wajanja.
    Walio juu wamejisahau kuwa kuna watu hata mlo mmoja hawana.
    Pato la Taifa ni kwao wao na familia zao na si haki ya kila mwananchi.
    Ulaya na Marekani shule ni bure (primary to high school including breakfast na lunch)na mtoto kama hajaenda shule mzazi unashitakiwa na kupelekwa mahakani.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...