Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi wa Kanda ya Mashariki na Kusini ya Afrika wa UNAIDS na Mwenyekiti wa High Level Group Profesa Sheila Tlou wakati wa ufunguzi wa mkutano wa High Level Group unaofanyika Cape Town nchini Afrika Kusini tarehe 6.12.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akihutubia mkutano wa siku mbili wa High Level Group, unaofanyika huko Cape Town tarehe 6 na 7, Desemba 2013. Mkutano huo unazungumzia masuala ya elimu na afya kwa vijana wanaoishi katika nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na viongozi wengine wa High Level Group wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwenye mkutano huo. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Kanda wa UNAIDS, Profesa Sheila Tlou na kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Jumuia ya Afrika Mashariki Mheshimiwa Jesca Eriyo.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akihutubia mkutano wa siku mbili wa High Level Group, unaofanyika huko Cape Town tarehe 6 na 7, Desemba 2013. Mkutano huo unazungumzia masuala ya elimu na afya kwa vijana wanaoishi katika nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimpongeza kijana Remmy Shawa, mjumbe wa High Level Group mara baada ya kutoa mada yake 'Background to the East and Southern Africa Commitment Process' kwenye mkutano wao wa siku mbili unaofanyika Cape Town nchini Afrika Kusini tarehe 6.12.2013. PICHA NA JOHN LUKUWI
Kwa habari kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Huyu mama nampenda kwa namna anavyoiwakisha nchi yetu vizuri.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...