Na Abdulaziz Video,Lindi Katika kulinda na kutetea ikiwemo kuendeleza maslahi ya mwanachama wa Mifuko ya hifadhi ya jamii Nchini,Mamlaka ya Usimamizi wa sekta ya Hifadhi za Jamii(SSRA)Imetoa mafuno kwa viongozi na waajiri Mkoani Lindi ili kutekeleza sheria iliyounda mamlaka hiyo na kuhakikisha huduma bora zinamfikia kila Mtanzania 
Akifungua mafunzo hayo,Mkuu wa Mkoa wa Lindi Ludovick Mwananzila kuwa Serikali inaandaa utaratibu maalumu utakaowawezesha wanachama wa mfuko husika kunufaika nao wakiwa kazini ama baada ya kumaliza utumishi wao. 
 Pia amewasisitizia wafanyakazi nchini kuwa suala hilo limepewa kipaumbele ili kupatiwa ufumbuzi haraka iwezekanavyo. Huku akiwasihi wafanyakazi wenye mawazo ya kuacha kazi ili tu wachukue mafao yao ya kujitoa kuachana na fikra hizo potofu ambazo alisema zitaleta athari kwa familia zao. Pamoja na Rai hiyo Mwananzila aliwataka SSRA kuhamasisha Mifuko ya Hifadhi za Jamii kutembelea mara kwa mara wanachama wao ikiwemo kutoa elimu ya mafao/Mikopo ambapo kufanya hivyo kutasaidia watumishi kujipanga baada ya kustaafu kuliko sasa mtumishi anachukia kustaafu 
“Jamani tunashuhudia wengi wanaona kustaafu ni kukaribia kifo na utumia mbinu nyingi kukwepa hilo kumbe kupitia Mifuko hii sasa ni mkombozi wa maisha ya wastaafu ila ni wazi kuna mifuko mingine ni kandamizi kwa mstaafu na haitoi fursa kwa mtumishi kushawishika kujiunga….”Alimalizia Mwananzila.
 Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano wa mamlaka hiyo Sarah Kibonde Msika akitoa mada katika mafunzo hayo alieleza kuwa SSRA imetoa miongozo sita (6) kwa lengo la kuhakikisha sekta ya hifadhi ya Jami inakuwa bora na endelevu itakayo boresha wanachama wa sekta ya hifadhi ya jamii kama ilivyoainishwa kwenye sheria na kufafanua kuwa miongozo hiyo pia itasaidia kuhakikisha mwanachama anapata haki yake anayostahili kwa wakati muafaka na kuondoa migongano baina ya mifuko,waajiri na waajiriwa. 
Pia Miongozo hiyo itahakikisha uwekezaji wa mifuko unaleta maendeleo bila kuhatarisha afya ya mifuko na utawala bora unaziongatiwa katika shughuli zote za uwekezaji kwa manufaa ya mifuko,wanachana na Taifa kwa Ujumla. 
‘Mamlaka inategemea kuwa katika kipindi kijacho sekta ya hifadhi ya jamii itakuwa endelevu,yenye mafao bora na mifuko ya hifadhi ya jamii itaongezeka. Kwa kuwa mamlaka inao uwezo wa kuchukua hatua za kinidhamu ikiwa pamoja na kutoa adhabu kwa wasimamizi na wadhamini wa mifuko kwa kutotekeleza matakwa ya sheria”Alieleza Kibonde alipokuwa anamalizia mada yake Mada nyingine katika Mafunzo hayo iliwasilishwa na Mkurugenzi wa Sheria SSRA,Bw Ngabo Patrick ambapo alieleza mafanikio na changamoto pamoja Muelekeo wa SSRA Ikiwa pamoja na kuendelea na mpango wa kuwianisha na kuhuisha mifuko ya hifadhi ya jamii ili kuhimiza wanajamii wengi zaidi kuingia katika mfumo wa hifadhi za jamii na kutopoteza haki zao pale inapobidi kuondoka katika mifumo hiyo 
Mafunzo ya Siku moja yamefanyika mjini Lindi ambapo pia baadhi ya Changamoto ilibainika ni vema Elimu Hiyo pia ikifikishwa kwa watumishi wa kada ya chini kupitia Mifuko ya Hifadhi pamoja na Mamlaka hiyo
 Mkuu wa Mkoa wa Lindi akifungua Mafunzo kulia ni Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Lindi Abdul Dachi na kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Sheria SSRA,Ngabo Patrich
 Baadhi ya Viongozi wakisiliza Mada zilizokuwa Zikiwasilishwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta za Hifadhi za jamii katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi
 Mkuu wa mawasiliano na uhamasishaji,Bi Sarah Kibonde Msika akiwasilisha mada kuhusiana na malaka ya SSRA
 Katibu wa Tughe Mkoa wa Lindi,Bi Frola Urassa akitaka apewe Ufafanuzi kuhusiana na Tofauti ya mafao yanayotolewa na mifuko ya Jamii
Mkuu wa Mkoa wa Lindi Ludovick Mwananzila akiwa katika Picha ya pamoja na watumishi wa Ofisi yake pamoja na watumishi wa SSRA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...